Wednesday, October 14, 2015
UMOJA WA MATAIFA WAANZISHA MIAKA 70 TANGU KUANZISHWA.
Do you like this story?
Waziri
wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mh Benard Membe amesema changamoto
kubwa inayoikabili umoja wa mataifa ni namna ya kusaidia athari zinazotokana na
wakimbizi katika nchi husika pamoja na kufidia watu wanaoathiriwa na wakimbizi.
Mh Membe
ameyasema hayo jijini Dar es Salaam kwenye maadhimisho ya miaka sabini ya umoja
wa mataifa ambapo amesema kwa sasa duniani kuna wakimbizi milioni 38 na
Tanzania imepokea wakimbizi 169,484 hivi karibuni na kwamba wanapoingia athari
ziko nyingi ikiwemo mashule kufungwa ili waweze kuhifadhiwa.
Rais mstaafu wa
awamu ya tatu Benjamin Mkapa akizungumza katika maadhimisho hayo amesema
uongozi na utawala bora umechangia kwa kiasi kikubwa Tanzania kuendelea kuwa
kisiwa cha amani na kuongeza kuwa kwa sasa nchi za Afrika zinafanya jitihada
kuhakikisha zinadumisha amani ili kuepuka kuzalisha wakimbizi.
Baadhi ya
viongozi wa dini waliohudhuria maadhimisho hayo wametoa wito kwa tume ya taifa
ya uchaguzi kusimamia haki na uadilifu ili Tanzania ibaki kisiwa cha manai hata
baada ya uchaguzi na kuwataka watanzania hasa vijana kufuata sheria kipindi
hiki ambacho nchi inakabiliwa na zoezi la uchaguzi mkuu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “UMOJA WA MATAIFA WAANZISHA MIAKA 70 TANGU KUANZISHWA.”
Post a Comment