Wednesday, October 14, 2015
.RAIS KIKWETE AITAKA TANESCO KUWASHA MITAMBO YOTE ILI KUPATA UMEME WAKUTOSHA.
Do you like this story?
Serikali kupitia TANESCO
imekamilisha miradi mitano na inatekeleza miradi mingine saba ya kufua umeme
kwa kutumia nishati ya gesi asilia mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara na
Lindi.Kiasi cha umeme unaofuliwa kwa kutumia gesi asilia unafikia megawati 546
na miradi iliyopo kwenye utekelezaji itakapokamilika inatarajiwa kuongeza
ufuaji wa umeme kutokana na gesi asilia kufikia megawati 2,475.Miradi hii
ipo kwenye hatua mbalimbali.
Leo Octoba 13 Tanesco ilizindua rasmi mradi
huo wa Umeme unaozaliwa kutokana na gesi asilia ambapo katika uzinduzi huo
mgeni rasmi alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Jakaya
Mrisho Kikwete.
Kukamilika
kwa miradi hiyo kutakidhi mahitaji ya umeme nchini na kuondoa utegemezi wa
mitambo ya kufua umeme kwa njia ya maji ambayo kiwango cha ufuaji wa umeme
kimeshuka kutokana na kushuka kwa kina cha maji kwenye mabwawa, hali ambayo kwa
kiwango kikubwa imesababishwa na mabadiliko ya tabia ya nchi pamoja na
kuendelea kwa shughuli za kibinadamu kwenye mito inayotiririsha maji kwenye
mabwawa hayo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “.RAIS KIKWETE AITAKA TANESCO KUWASHA MITAMBO YOTE ILI KUPATA UMEME WAKUTOSHA.”
Post a Comment