Saturday, October 31, 2015
UPDATES: NDEGE YA URUSI YENYE WATU 224 ILIYOANGUKA SINAI, MISRI LEO
Do you like this story?
Ndege ya Shirika la Kogalymavia la Urusi, Airbus A-321 iliyoanguka eneo la Sinai nchini Misri |
Muonekano wa Jangwa la Sinai ambako ndege hiyo imeanguka. |
Waziri Mkuu wa Misri, Sharif Ismail akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani). |
Ndugu wa habiria waliokuwa katika ndege wakilia wakiwa katika Uwanja wa ndege wa wa St. Petersburg nchini Urusi. |
NDEGE ya Shirika la
Kogalymavia la Urusi, iliyowabeba abiria 200, watoto 17 na wafanyakazi wa ndege
hiyo 7, imeanguka katika eneo la Sinai nchini Misri, ofisi ya waziri mkuu wa
Misri imethibitisha.
Ndege hiyo aina ya Airbus A-321 ilikuwa
imetoka Mji wa Sharm el-Sheikh ikielekea mji wa St. Petersburg nchini Urusi
ilipoanguka.
Mili ya watu 100 walikufa wameondolewa eneo
la ajali na watoto 17 wamekutwa wakiwa hai.
Vyombo vya habari nchini Misri vinasema
mabaki ya ndege hiyo yamepatikana na magari 50 ya kubebea wagonjwa yametumwa
eneo la ajali.
Awali, kulikuwepo na utata kuhusu hatima ya
ndege hiyo, baadhi ya ripoti zikisema ilitoweka karibu na Visiwa vya Cyprus.
Lakini ofisi ya Waziri Mkuu wa Misri, Sharif Ismail amethibitisha kwamba ndege
hiyo ilianguka katikati ya eneo la Sinai.
Waziri Mkuu wa Misri, lsmail ameunda kamati
ya dharura ya kushughulikia ajali hiyo.
Shirika la Urusi linalosimamia safari za
ndege, Rosaviatsiya limesema ndege hiyo iliyokuwa katika safari nambari 7K 9268
iliondoka Sharm el-Sheikh saa 06:51 saa za Moscow (0:351 GMT) na ilitarajiwa
kuwasili Uwanja wa Ndege wa Pulkovo mjini St Petersburg saa 12:10 leo.
Ndege hiyo ilikosa kuwasiliana na wasimamizi
wa safari za ndege Cyprus dakika 23 baada ya kupaa kama ilivyoratibiwa na
ikatoweka kutoka kwenye mitambo ya rada.
Kituo maalum kimefunguliwa Uwanja wa Ndege wa
Pulkovo kusaidia abiria waliokuwa kwenye ndege hiyo, shirika la habari la Tass
limesema likinukuu maafisa wa Jiji la St Petersburg.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “UPDATES: NDEGE YA URUSI YENYE WATU 224 ILIYOANGUKA SINAI, MISRI LEO”
Post a Comment