Tuesday, March 15, 2016
POLISI DAR YAKAMATA MAGARI 24 YA WIZI NA DADA & KAKA POA 287
Do you like this story?
Jeshi la Polisi kanda
maalumu ya mkoa wa Dar es Salaam imeendesha oparesheni kali dhidi ya uhalifu
mbalimbali na kufanikiwa kukamata watu 287 wenye kujihusisha na masuala ya
kuuza miili yao (dada poa na kaka poa), magari 24 ya wizi huku likifanikiwa
kukamata mtandao wa watu wenye kujihusisha na wizi wa magari kutoka Dar es
Salaam na kuyapeleka mikoa ya kanda ya ziwa
Akizumgumzia
mafanikio ya oparesheni hiyo Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya mkoa wa Dar es
Salaam, Kamishina simon Sirro alisema jeshi hilo limekuwa likiendelea na
utekelezaji wa majukumu yake ya kikazi ambapo safari hii limefanikiwa
kuwakamata watu 287 wenye kujihusisha na biashara ya kuuza miili yao jambo
ambalo ni kinyume na maadili ya mila za kitanzania.
Kamishna Sirro
ameongeza kuwa kuwa licha ya jeshi hilo kuwakamata watu hao kutoka Temeke,
Kinondoni na Ilala, jeshi hilo limefanikiwa kuyakamata magari 24 yanayotokana
na wizi ambao pia mtandao wake umeweza kubainika na watuhumiwa 50 wamekamatwa.
“Tumefanikiwa
kukamata watuhumiwa mbalimbali ambao wanajihusisha na vitendo vya uharifu kwa
kuiba magari na kusafirisha kwenda mikoani na uchunguzi zaidi unaendelea ili
kuwabaini wote wanaojihusiha,” alisema Kamanda Sirro.
Aidha Kamishna Sirro
aliwatoa hofu wakazi wa Dar es Salaam juu ya hali ya usalama kwani jeshi hilo
limejipanga vilivyo na kuwataka waendelee kuwa raia wema kwa kutoa taarifa za
ualifu kwa vyombo vya usalama ili ziweze kufanyiwa kazi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ POLISI DAR YAKAMATA MAGARI 24 YA WIZI NA DADA & KAKA POA 287”
Post a Comment