Tuesday, November 1, 2016
WANAFUNZI WAPIGWA RADI WAKATI WAKILA CHAKULA SHULENI MAKETE.
Do you like this story?
Jumla ya wanafunzi 10 wa shule ya sekondari Mang'oto Kata
ya Mang'oto wilayani Makete mkoani Njombe wamejeruhiwa na radi baada ya Mvua
iliyoambatana na radi kunyesha shuleni hapo na kuwapiga wanafunzi hao
Akizungumza na Mwandishi wa eddy blog shuleni hapo Mkuu
wa shule hiyo Mwl. Bonaventura Mgaya (pichani juu) amesema tukio hilo limetokea
Oktoba 30 mwaka huu majira ya saa saba na nusu mchana wakati wanafunzi wakipata
chakula cha mchana shuleni hapo
Amesema radi hiyo ilivyopiga wanafunzi wengi walidondoka
chini hali iliyowafanya walimu kwenda kuwasaidia na baada ya dakika chache
baadhi yao waliweza kuzinduka ndipo walimu walipofanya uchunguzi wa awali
kugundua majeruhi na kuwakimbiza kupata huduma za afya katika zahanati ya
Mang'oto
Uchunguzi wa wataalamu wa afya katika zahanati hiyo
ulibaini mtoto mmoja kujeruhiwa zaidi upande wa kulia wa mwili wake kuanzia
begani mpaka mapajani na kulazimika uongozi wa shule kumkimbiza mpaka hospitali
ya Consolata Ikonda kwa matibabu zaidi, kabla ya baadaye wanafunzi wengine
watatu walioonekana awali kuwa walikuwa na nafuu walizidiwa na kukimbizwa tena
katika hospitali hiyo kwa matibabu zaidi
Mwalimu Mgaya pia amezungumzia madhara mengine
yaliyotokana na radi hiyo kuwa ni kuunguza mfumo wa umeme wa sola uliokuwa ukitumika
shuleni hapo, na mpaka tunakwenda mitamboni shule hiyo haina umeme kwa sasa
Mmoja kati ya wanafunzi waliopigwa na radi hiyo Manfred
Mwageni anayesoma kidato cha kwanza shuleni hapo akielezea tukio hilo amesema
alishangaa kujikuta ametupwa chini na radi hiyo huku ikiwaunguza wanafunzi
wengine
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ WANAFUNZI WAPIGWA RADI WAKATI WAKILA CHAKULA SHULENI MAKETE.”
Post a Comment