Tuesday, November 1, 2016

KIGOGO ALIYELAMBA FEDHA ZA SERIKALI ASHTAKIWA KWA MAKOSA 330





Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU imempandisha mahakamani kigogo mmoja wa mamlaka ya elimu nchini TEA  Bw. Isaya Paul kwa makosa 330 ambayo yameisababishia serikali hasara ya zaidi ya shilingi milioni  560.

Kigogo huyo ambaye amepandishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Kinondoni mbele ya hakimu mfawidhi Frank Moshi  amesomewa mashtaka hayo  na wanasheria wawili kutoka TAKUKURU Bi .Faraja Samale na Bi. Vero Ndeoya ambao katika mashtaka hayo wameiambia  mahakama kuwa katika nyakati na tarehe tofauti kwa mwaka 2011 na 2013  mshtakiwa huyo aliiba fedha za serikali kupitia benki ya CRDB  tawi wa Kijitonyama wakaongeza kuwa mtuhumiwa huyo alifanya hivyo akijua wazi kuwa ni kosa kisheria  na hasa kwa yeye ambaye ni mtumishi wa umma mwenye dhamana kubwa ya kutunza na kufanya matumizi sahihi ya fedha ambazo zilikuwa ndani ya dhamana  yake  yeye.

Aidha mahakama ikaambiwa kuwa mtuhumiwa huyo mbali na kufanya wizi kupitia  benki hiyo ya CRDB pia kwa nyakati tofauti tofauti  katika maeneo yasiyojulikana amekuwa akighusihi  hundi mbalimbali za mamlaka ya elimu nchini  na kujipatia fedha  kwa kudai  kuwa hundi hizo ni halali akiwa kama mfanyakazi wa mamlaka hiyo.

Mshitakiwa huyo amekana makosa yote 330 ambapo kupitia wakili   anayemtetea  Bw .Agustino Kusalikwa ameiomba mahakama kumpatia dhamna mteja wake huyo lakini hakimu Mh. Moshi  akasema kwa mujibu wa sheria kwa kosa ambalo linahusisha fedha  zaidi ya shilingi milioni kumi mahakama hiyo haina uwezo wa kutoa dhamana na hivyo mshtakiwa yupo ndani hadi novemba 14  mwaka huu.

0 Responses to “ KIGOGO ALIYELAMBA FEDHA ZA SERIKALI ASHTAKIWA KWA MAKOSA 330”

Post a Comment

More to Read