Tuesday, November 1, 2016
KIGOGO ALIYELAMBA FEDHA ZA SERIKALI ASHTAKIWA KWA MAKOSA 330
Do you like this story?
Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU imempandisha mahakamani kigogo mmoja
wa mamlaka ya elimu nchini TEA Bw. Isaya Paul kwa makosa 330 ambayo
yameisababishia serikali hasara ya zaidi ya shilingi milioni 560.
Kigogo
huyo ambaye amepandishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Kinondoni mbele ya
hakimu mfawidhi Frank Moshi amesomewa mashtaka hayo na wanasheria
wawili kutoka TAKUKURU Bi .Faraja Samale na Bi. Vero Ndeoya ambao katika
mashtaka hayo wameiambia mahakama kuwa katika nyakati na tarehe tofauti
kwa mwaka 2011 na 2013 mshtakiwa huyo aliiba fedha za serikali kupitia
benki ya CRDB tawi wa Kijitonyama wakaongeza kuwa mtuhumiwa huyo alifanya
hivyo akijua wazi kuwa ni kosa kisheria na hasa kwa yeye ambaye ni
mtumishi wa umma mwenye dhamana kubwa ya kutunza na kufanya matumizi sahihi ya
fedha ambazo zilikuwa ndani ya dhamana yake yeye.
Aidha
mahakama ikaambiwa kuwa mtuhumiwa huyo mbali na kufanya wizi kupitia
benki hiyo ya CRDB pia kwa nyakati tofauti tofauti katika maeneo
yasiyojulikana amekuwa akighusihi hundi mbalimbali za mamlaka ya elimu
nchini na kujipatia fedha kwa kudai kuwa hundi hizo ni halali
akiwa kama mfanyakazi wa mamlaka hiyo.
Mshitakiwa
huyo amekana makosa yote 330 ambapo kupitia wakili anayemtetea Bw
.Agustino Kusalikwa ameiomba mahakama kumpatia dhamna mteja wake huyo lakini
hakimu Mh. Moshi akasema kwa mujibu wa sheria kwa kosa ambalo linahusisha
fedha zaidi ya shilingi milioni kumi mahakama hiyo haina uwezo wa kutoa
dhamana na hivyo mshtakiwa yupo ndani hadi novemba 14 mwaka huu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ KIGOGO ALIYELAMBA FEDHA ZA SERIKALI ASHTAKIWA KWA MAKOSA 330”
Post a Comment