Friday, May 26, 2017

AUDIO: Mwanafunzi auawa Makete, Kisa akutwa akiokota Kuni


 Mwilli wa mwanafunzi huyo ukiondolewa katika hospitali ya Consolatha Ikonda hii leo

Mwanafunzi Jetrida Sanga wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Ukwama wilayani Makete mkoani Njombe amevamiwa na  mtu asiye fahamika na kusababisha kifo chake wakati akiokota kuni jana na wanafunzi wenzake katika pori la Luhenye lililopo kijiji cha Ukwama wilayani hapo.
Miongoni mwa Mashuhuda wa tukio hilo ambao ni wanafunzi wenzake na marehemu wamelezea namna tukio hilo lilivyotokea huku wakidai kuwa wakati wanaendelea kuokota kuni alijitokeza mtu wa jinsi ya kiume ambaye aliwauliza kwa nini wanaokota kuni zake msituni humo, na ghafla akanza kufanya kumvamia mwanafunzi huyo

Sikiliza Taarifa hii ya kina kama ilivyoripotiwa na kituo cha Redio Green FM 91.5 kilichopo wilayani Makete kwa kubonyeza play hapo chini

0 Responses to “AUDIO: Mwanafunzi auawa Makete, Kisa akutwa akiokota Kuni ”

Post a Comment

More to Read