Wednesday, September 13, 2017
Picha: Makamu wa Rais azindua programu ya maboresho ya usimamizi wa fedha za umma
Do you like this story?
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mhe. Samia Suluhu
Hassan akisalimiana na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Philip Mpango
wakati akiwasili kwenye uzinduzi wa Programu ya Maboresho ya Usimamizi
wa Fedha za Umma Awamu ya Tano 2017/18 – 2021/22 katika Ukumbi wa Hazina
mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu
Hassan akihutubia wakati uzinduzi wa Programu ya Maboresho ya Usimamizi
wa Fedha za Umma Awamu ya Tano 2017/18 – 2021/22 katika Ukumbi wa Hazina
mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu
Hassan akizindua Programu ya Maboresho ya Usimamizi wa Fedha za Umma
Awamu ya Tano 2017/18 – 2021/22 kulia ni Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.
Philip Mpango ambapo pia ilishuhudiwa na Spika wa Bunge wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai, Spika wa Baraza la Wawakilishi
Mhe.Zubeir Ali Maulid, Naibu Waziri Ofisi ya Rais,TAMISEMI Mhe. Selemani
Jaffo, Naibu Waziri Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji na Wadau wa
Maendeleo kwenye Ukumbi wa Hazina mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya
Makamu wa Rais)
Sehemu ya Waliohudhuria wakipiga makofi mara baada ya Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan kuzindua
Programu ya Maboresho ya Usimamizi wa Fedha za Umma Awamu ya Tano
2017/18 – 2021/22 katika Ukumbi wa Hazina mjini Dodoma. (Picha na Ofisi
ya Makamu wa Rais)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “Picha: Makamu wa Rais azindua programu ya maboresho ya usimamizi wa fedha za umma”
Post a Comment