Wednesday, September 13, 2017
Bunge limefunguliwa Kenya, upinzani umesusia
Do you like this story?
Rais wa Kenya Uhuru
Kenyatta amewataka wabunge kuheshimu katiba wakati wa kufunguliwa bunge
kwenye kikao chake cha kwanza tangu ufanyike uchaguzi wa tarehe 8
Agosti.
Rais Kenyatta alisema kuwa kipindi hiki ambacho Kenya
inasubiri kurudiwa kwa uchaguzi uliofutwa na mahakana, ni muhumu kwa
katiba kuheshimiwa.
Alirejelea matamshi yake kuwa hakubaliani na
uamuzi wa mahakama ya juu wa mwezi uliopitawa kufuta matokeo ya urais,
lakini alikubali kwa sababu anaheshimu katiba.
Lakini Kenyatta alisema kuwa hadi pale rais mpya ataapishwa yeye bado ni rais.
Wabunge kutoka muungano upanzani Nasa hawakuwa bungeni kwa
sababu wanapinga kikao hicho wakisema kuwa bado nchi inasubiri kufanya
marudio ya uchaguzi.
Wakati wa kufunguliwa kwa bunge NASA nao
walikuwa wakiendelea na mkutano wao katika ngome yao kisiasa, mtaa wa
Kibera mjini Nairobi.
Bunge linafunguliwa huku wakenya wakijiandaa tena kupiga kura tarehe 17 mwezi Oktoba.
Mahakama
ya juu zaidi nchini Kenya iliamrisha uchaguzi wa urais kurudiwa kutoka
na hitilafu zilizotokea kwenye uchaguzi mkun uliofanyika tarehe 8 mwezi
Agosti.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “Bunge limefunguliwa Kenya, upinzani umesusia”
Post a Comment