Wednesday, September 13, 2017
Manchester United yarejea kwa kishindo UEFA
Do you like this story?
Manchester United imeanza
vyema michuano ya UEFA Klabu Bingwa Ulaya kwa kuizaba FC Basel kwa mabao
3-0. Mchezo huo wa kwanza wa kundi A ulichezwa kwenye uwanja wa Old
Trafford.
Bao la kwanza lilifungwa na Maroanne Fellaini ambaye
alingia badala ya Paul Pogba aliyetoka kutokana na kujeruhiwa. Marcus
Rashford ambaye alin'gara katika michuano ya Kombe la Europa, alianza
michuano ya Ulaya kwa kufunga bao la tatu. Mchezo mwingine wa Kundi A
ulikuwa kati ya Benfica na CSKA Moscow, ambapo wageni waliibuka na
ushindi wa mabao mawili kwa moja.
Mabingwa wa England Chelsea nao walianza michuano
hii kwa kutoa kisago cha nguvu baada ya kuichapa FC Qarabag kwa magoli
6-0 kwenye mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Stamford Bridge, London.
magoli ya Chelsea yalifungwa na Pedro (dk 5), Zappacosta (dk 30),
Azpilicueta (dk 55), Bakayoko (dk 71), Batshuayi (dk 76 na 82).
Kwingineko
Paris Saint- Germain iliizaba Celtic mabao matano kwa sifuri, Neymar,
Kylian Mbappe na Edinson Cavani wakicheka na nyavu katika mchezo wa
kundi B. Bayern Munich pia walipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya
Anderlecht.
Barcelona pia ilianza vizuri kwa kuichapa Juventus
kwa magoli 3-0, Messi akifunga mawili na Ivan Rakitic la tatu. Sporting
Lisbon wakicheza ugenini walipata ushindi wa 3-2 dhidi ya Olympiakos.
Mcezo pekee uliomalizika bila magoli ulikuwa kati ya Roma dhidi ya
Atletico Madrid.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “Manchester United yarejea kwa kishindo UEFA”
Post a Comment