Wednesday, September 6, 2017
WAFANYABISHARA SOKO LA SIDO WARUHUSIWA KUENDELEA NA UJENZI
Do you like this story?
Mkuu Wa Wilaya ya Mbeya Mh,Paul Ntinika akizungumza na wafanyabiashara wa soko la Sido juu ya uanzaji wa ujenzi ndani ya mwezi mmoja |
Wafanyabiashara wa soko la Sido wakimsikiliza Mkuu Wa Wilaya ya Mbeya katika mkutano uliofanyika leo katika viwanja vya sido |
Baadhi ya wafanyabiashara wakiuza biashara zao katika soko la sido baada ya mkuu wa wilaya kuruhusu ujenzi kuanza |
Wafanyabiashara wa soko la sido wakianza ujenzi mara baada ya tamko la Mkuu Wa Wilaya kuwaruhusu kujenga katika mpangilio wa umepangwa na jiji |
SERIKALI Mkoani hapa imetoa muda wa
mwezi mmoja kwa wafanyabiashara wa soko la Sido jijini Mbeya,kuhakikisha
wanakamilisha Ujenzi wa vibanda, ikiwa ni siku saba tangu itangaze kusimamisha
kwa muda usiyo julikana kwa kile kilicho elezwa kuwa mchoro wa soko hilo
haukudhibitishwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
Mbali ni kuruhusiwa kuendelea na
ujenzi lakini pia Serikali imetangaza kuwa Ujenzi wa soko hilo utafanyika kwa muda
wa mwezi Mmoja kuanzia Septemba 6 mwaka huu na baada ya hapo wafanyabiashara
wote wataruhusiwa kuanza biashara bila kulipa Ushuru wa soko kwa muda wa miezi
sita.
Akitangaza uamuzi huo mbele ya
wafanyabiashara na wahanga wa moto,kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos
Makalla, Mkuu Wilaya ya Mbeya Wiliam Paul Ntinika amesema kuwa uamuzi huo umeamliwa
na kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa kwa kuzingatia maslahi mapanaa ya
wafanyabishara hao na Taifa kwa ujumla.
Amesema kuwa mbali na kuzingia
maslahi mapana ya taifa lakini pia kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa iliyafanyia
kazi na kuyazingatia maombi ya wafanyabiashara hao yaliyowasilishwa na viongozi
wao ya kutaka wabaki eneo hilo lakini pia Serikali iharakishe kutoa ramani ili
watu waweze kuendelea na Ujenzi.
Aidha Ntinika amewataka wafanyabishara
kutoa ushrikiano kwa watalaamu kutoka Idara ya Mipango Miji,Shirika la Umeme
Tanesco,Zimamoto ambao wapo kwa ajili kusimamia na kutoa ushauri wa kitaalumu
wakati wote wa Ujenzi wa soko hilo ambalo Agost 15 mwaka huu liliteketea kwa
moto.
Hata hivyo Serikali imewaruhusu
kuendelea na Ujenzi kwa mara nyingine ikiwa ni siku saba tangu iwatake
wafanyabishara kusimama kwa kile kilichokelezwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya
haikudhibitisha mchoro huo, na Zuio hilo linakuja ikiwa ni siku chache tangu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla afanye
Mkutano na kuwaruhusu kuendelea na ujenzi wa vibanda vya kudumu,katika soko hilo.
Naye mwenyekiti wa Jumuhiya ya
wafanyabishara mkoa wa Mbeya, Charlers Syonga ameishukuru serikali kwa
kusikiliza kilio cha wafanyabiashara na hatimaye kufikia uamuzi kuwaruhusu wafabiashara
kuendelea kubaki katika eneo hilo la sido
Naye Gibons Bukuku mfanyabiashara
katika soko hilo na mwenye Ulemavu wa miguu ambaye ni muhanga wa tukio la Moto
ameishukuru Serikali kwa uamuzi wa kuwarejesha katika eno hilo huku akitaka
Serikali ilisimamie ujenzi kwa kuweka miundombinu rafiki rafiki kwa watu wenye
Ulemavu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WAFANYABISHARA SOKO LA SIDO WARUHUSIWA KUENDELEA NA UJENZI ”
Post a Comment