Wednesday, March 19, 2014
RAIS ZUMA ALIFUJA PESA ZA UMMA?.
Do you like this story?
Mkuu wa idara ya kupokea malalamishi
ya umma, Bi Thuli Madonsela hivi leo anatarajiwa kutoa ripoti ya idara hiyo
kuhusu uchunguzi wa iwapo Rais Jacob Zuma alihusika katika ufisadi.
Rais huyo wa Afrika Kusini inadaiwa
alitumia pesa za umma dola milioni ishirini kukarabati boma lake la kifahari
lililopo katika kijiji cha Nkandla alikozaliwa.
Vyombo vya habari nchini Afrika
Kusini vimedokeza kuwa Rais Jacob Zuma amefanya mashauriano na Bi Madonzela,
hivi karibuni wakati ambapo chama tawala cha ANC kimetoa wito kwa wanachama
wake kupuuza repoti hiyo ya Bi Madonzela iwapo itamshirikisha Rais Zuma.
Boma la Nkandla la kibinafsi la Rais
Zuma lina nyumba kadhaa, na limewekwa mitambo ya kisasa ya kiusalama ili
kumlinda Rais.
Kulingana na mwandishi wa BBC wa
Afrika Kusini, Omar Murtasa, Waziri wa Ujenzi wa Kazi za Umma nchini humo
Nthula Tsinthesi, ilikuwa muhimu kukarabati boma hilo kwa kiasi hicho cha pesa
kwa sababu boma hilo limewahi kuvamiwa mara tatu na wahalifu.
Ukarabati huo wa boma la Rais ambao
sasa umenukia kuwa kashfa umewafanya wengi kuhoji iwapo bwawa la kuogelea la
kisasa lililojengwa kwa kiasi kikubwa cha pesa ni sehemu ya usalama unaotajwa.
Na pia kumekuwepo na habari
zinazodaiwa kuwa katika ripoti hiyo ambazo zinadai kuwa Rais Zuma mwenyewe
alitoaamri pesa za umma kutumiwa,
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “RAIS ZUMA ALIFUJA PESA ZA UMMA?.”
Post a Comment