Wednesday, March 19, 2014
WARIOBA AWAKUNA WASOMI, WACHAMBUZI.
Do you like this story?
baadhi ya wasomi na wachambuzi
wa masuala ya kisiasa hapa nchini wamesema
hotuma ya mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba jaji joseph warioba
itasaidia kubadilisha msimamo wa wajumbe wengi
wa bunge maalumu la katiba.
Kauli hiyo imekuja muda
mfupi baada ya jaji warioba kuwasilisha rasimu ya pili ya katiba katika bunge
hilo tayari kwa kuijadili kuiboresha na
hatimaye kutoka na rasimu tatu itakayopigiwa kura ama kuikubali kuwa katiba mpya au la.
Mwanasiasa mkongwe njelu
kasaka amesema hotuba hiyo imesaidia
kutoa uelewa wa mambo kwa kuwa idadi
kubwa ya wajumbe ndani ya bunge hilo hawakuwan na uelewa juu ya hoja
mbalimbali zilizopendekezwa kwenye rasimu hiyo.
Kutokana na ufafanuni huo
wengi watakuwa wameelwa kwa nini tume iliamua kupendekeza muungano wa serikali
tatu na wala siyo mbili. Itasaidia pia kuwajengea uwezo wa kuhoji kaatika
mijadala ya kamati itakapoanza kukaa rasmi alisema kasaka ambye alikuwa
miongoni mwa wabunge 55 walioasisi kundi
la G55 lililotaka kuundwa serikali ya Tanganyika mwaka 1993.
Lakini jambo jingine
hotuba hii imeondoa ni unafiki na
imewaaibisha kwa unafiki wao baadhi y a watu kwa sababu pamoja na kuongoza
serikali moja ya jamhuri ya muungano , imefahamika wazi kwamba waziri mkuu
kumbe hana mamlaka yoyote yale katika upende wa Zanzibar.
Kwa upande wake profesa
boniventure rutinwa wa chuo kikuu cha dar es salaam(UDSM) aliunga mkono hoja
hiyo akisema kinachotakiwa kwa wajumbe
hao ni kujenga imani, kuondoa tofauti zao na kutokubaliana na hoja zenye
masilahi ya vyama na makundi yao badala ya Taifa.
Kinachotakiwa kwa sasa ni
kupima uwezo wa kwa kuhoji je pamoja na
ufafanuzi huo serikali tatu inaweza kuwa
mwarobani wa kumaliza changomoto zote? Lakini pia wanatakiwa kufahamu kwamba
inawezekana kuna changamoto nyingine ambazo zinaweza jitokeza katika muundo huo. Alisema profesa rutinwa.
Kwa upande wake profesa
penina mlama aliwataka wajumbe wa bunge hilo kuchukua hoja hizo na kufikiria
kwa mapana zaidi wakati wa majadiliano ili kuondoa athari zinazoweza kujitokeza
baadaye.
Wamerahisishiwa na kazi
imebakia kwao kupima na kufikiria zaidi
hotuba hii wajumbe watambue kwamba si
mawazo ya jaji warioba yaliyowasilishwa pale pale ni amwazo ya watanzania ambayo
yanatakiwa kupokew kwa mtanzamo chanya ili wasije kuaibika badaye iwapo watashindwa kufanya uamuzi
sahihi alisema.
Mjumbe wa bunge james
mapalala alisema jaji warioba amemaliza kazi ya kuelimisha juu ya umuhimu wa serikali tatu na anamini
wataosimama kumpinga wataona haya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WARIOBA AWAKUNA WASOMI, WACHAMBUZI.”
Post a Comment