Tuesday, April 22, 2014
HUU NI UKATILI NA UNYANYASAJI TAZAMA PICHA MTOTO AFUNGWA KAMBA ASITOKE NYUMBANI KWAO.
Do you like this story?
Mtoto Samir mkazi wa mtaa wa Langoni kata ya Miembeni,akiwa
amefungwa kamba katika mguu wake wa kushoto huku upande mwingine ukiwa
umefungwa katika chuma kizito kilichopo jirani na mlango.
|
Na Dixon Busagaga
MTOTO Samir anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka minne hadi
mitano mkazi wa mtaa wa Langoni katika manispaa ya Moshi, amejikuta katika
wakati mgumu kutokana na tabia ya bibi yake kumfunga kamba katika mguu wake kwa
lengo la kumzuia asiende kucheza mbali na nyumbani kwao.
Tukio
hilo limetokea hivi karibuni katika eneo hilo ambapo bibi huyo ambaye jina lake
halikufahamika mara moja alikutwa akiwa amemfunga kamba ya kudu mjukuu wake
huyo katika mguu wa kushoto huku sehemu nyingine ikiwa imefungwa katika chuma
kizito.
Kwa mujibu wa majirani walisema bibi huyo amekuwa akimfunga
mtoto huyo mara kwa mara kwa zaidi ya nusu saa hasa nyakati ambazo bibi huyo
amekuwa akifanya shughuli zake za usafi wa ndani pamoja na kufua.
Wakizungumza kwa sharti la kutotajwa majina,majirani hao
wamesema imekuwa ni kawaida kwa bibi huyo ambaye anaishi na wajukuu zake
kumfanyia kitendo hicho mtoto huyo huku akimzuia kucheza na wenzake wa nyumba
za jirani.
“Sisi hiyo hali mbona tumeizoea mara kwa mara Samir akienda
kucheza na wenzake huko mtaani,bibi yake akimkuta huko anamkamata na kisha
kumfunga kwenye hilo chuma lililoko hapo mlangoni kwa zaidi hata ya nusu
saa”alisema mmoja wa majirani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “HUU NI UKATILI NA UNYANYASAJI TAZAMA PICHA MTOTO AFUNGWA KAMBA ASITOKE NYUMBANI KWAO.”
Post a Comment