Tuesday, April 22, 2014
POLISI MOROGORO YAFUATA NYAYO ZA MBEYA CITY FC.
Do you like this story?
BAADA ya
kurejea ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2014/2015, klabu ya Polisi
Morogoro ameanza tambo za kuja na muonekanao mpya.
Afisa habari
wa klabu hiyo, Clemence Banzo ameueleza mtandao huu kuwa wapo katika mikakati
mikubwa ya kuijenga timu yao kwa kusajili wachezaji chipukizi na kuimarisha
masuala ya utawala mithiri ya Mbeya City FC.
“Kiukweli
Mbeya City wametupa fundisho kubwa sana. Mafanikio yao yametugusa, na ipo haja
ya kuiga nyayo zao”.
“Kwanza
tunatarajia kufanya usajili usiojali majina kama wao. Pili tunaanza maandalizi
ya mapema ili kujiimarisha zaidi”. Alisema Banzo.
Banzo
aliongeza kuwa Polisi Moro ya sasa itakuwa tofauti na ya zamani kwasababu
wanataka kuipeleka zaidi kwa wananchi wa mkoa wa Morogoro.
‘Mashabiki ni
nguzo muhimu sana katika soka, angalia Mbeya City jinsi walivyo na nguvu
kwasababu ya watu wengi kuwa nyuma yao. Nasisi Polisi tunaona ipo haja ya
kuipeleka timu hii kwa wananchi”.
“Tunaanza
mchakato wa kufungua matawi maeneo tofauti nchini, lengo likiwa ni kuwa na
uhusiano wa karibu na mashabiki wetu”. Alisema Banzo.
Aidha, afisa
habari huyo alisema kuwa wamefanya kazi kubwa kurudi ligi kuu, hivyo wanataka
kufanya jitihada za kushiriki kwa muda mrefu.
“Ni rahisi
kushuka daraja, lakini kurudi ni changamoto kubwa. Tunamshukuru Mungu ndani ya
mwaka mmoja tumerudi ligi kuu, lakini changamoto iliyopo mbele yetu ni kuwa na
timu ya ushindani na si ushiriki”. Alisema Banzo.
Polisi
Morogoro ni moja ya timu tatu zilizopanda kushiriki michuano ya ligi kuu soka
Tanzania bara msimu wa 2014/2015.
Timu nyingine
ni Ndanda fc ya Mkoani Mtwara na Stand United ya shinyanga.
Timu
zilizoshuka daraja ni Rhino Rangers ya Tabora, JKT Oljoro ya Arusha na Ashanti
United ya Dar es salaam.
Ujio wa
Ndanda fc unatabiriwa kuwa mzuri kutokana na uzalendo wanaounesha mashabiki wa
soka mkoani Mtwara.
Baada ya timu
hiyo kupanda ligi kuu, mamia ya mashabiki walijitokeza kuipokea timu uwanja wa
ndege na kupanga foleni barabarani kuishangilia inapopita mitaani.
Baada ya hapo
walianzisha slogani ya `Ndanda fc kwa roho safi`, inayomaanisha wanaisapoti
timu yao kwanza na kuachana na Simba na Yanga.
Hata watu wa
Shinyanga wameonekana kuwa na furaha kubwa na timu yao kupata nafasi ya kucheza
ligi kuu, hivyo wanatarajiwa kuiunga mkono kama ilivyo kwa wakazi wa Mbeya.
Kama timu
hizi zitapata nguvu kama ya Mbeya City fc basi itakuwa changamoto
nyingine kwa timu za juu, Azam fc, Yanga na Simba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “POLISI MOROGORO YAFUATA NYAYO ZA MBEYA CITY FC.”
Post a Comment