Tuesday, February 25, 2014
54 WAKAMATWA KWA UNYWAJI WA POMBE SAA ZA KAZI JIJINI MBEYA
Do you like this story?
![]() |
Mfanyabiashara wa pombe za kienyeji akiwa katika harakati za kuuza majira ya saa tatu asubuhi |
![]() |
Vibanda vinavyotumika kwaajiri ya pombe za kienyeji |
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahamed Msangi | M |
Na David Nyembe, Mbeya.
LICHA ya Polisi Mkoani Mbeya, kufanikiwa kukamata watu 54 kwa
unywaji wa pombe saa za kazi, wakazi wa Jiji la Mbeya
wameliomba jeshi hilo kuvifungia vialabu vya pombe na kumbi za
starehe ambazo zitabainika kuendesha shughuli hizo nyakati za kazi.
Wakitoa kero hizo leo kwa mwakilishi wa Fahari News, baadhi ya
wakazi wa eneo la Mabatini, wamesema mwaka 2009 serikali kupitia sheria
ndogo za halmashauri ilifanikiwa kutekeleza zoezi hilo kwa kudhibiti unywaji wa
pombe saa za kazi kwa kuvifungia vilabu vya pombe, kumbi za starehe na mchezo
wa Pool Table.
Wamesema zoezi hilo
lilifanikiwa kwa asilimia 100 kwani mwananchi aliyebainika kukiuka sheria
hiyo aliwajibika kwa kulipa faini ya shilingi 50,000/= na wale walioshindwa
walifikishwa mahakamani.
“Unajua ndugu mwandishi vijana wetu wamekuwa wakitumia muda mwingi
kwa unywaji wa pombe, kuendekeza anasa kwenye kumbi za starehe pamoja na
kucheza mchezo wa pool table badala ya kufanya kazi mashambani,”amesema Joseph
Mwakambili mkazi wa Mabatini
Amesema, vijana wengi wamekuwa wakikimbia kazi mashambani huku
wakitambua njia pekee ya kuondokana na hali ya umaskini ni kujikita zaidi
kwenye sekta ya kilimo na mifugo kwani ndio nguzo pekee
itakayowatoa kwenye dimbwi la umaskini.
Mapema mwaka huu Polisi Mkoani Mbeya, kupitia zoezi la
ukamati wa watu ambao wanajihusisha na vitendo vya unywaji wa pombe saa
za kazi limefanikiwa kukamata watu 54.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Robert Mayala, amesema
watu hao walikamatwa katika matukio mawili tofauti ambapo
February 24 mwaka huu saa sita za mchana katika Mtaa wa
Ilemi walikamatwa watu 17 huku January 22 mwaka huu walikamatwa watu 37
Jijini Mbeya.
Hata hivyo, Mayala amewataka wakazi wa Mbeya kuheshimu na nidhamu
katika muda wa kazi si muda na kwamba si muda wote wakausudisha pombe na
kuendekeza starehe ambazo hazimsaidii mtu kuondokana na hali ya umaskini.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “54 WAKAMATWA KWA UNYWAJI WA POMBE SAA ZA KAZI JIJINI MBEYA”
Post a Comment