Wednesday, February 26, 2014
SIRI YA UFAULU WA ST FRANCES MBEYA
Do you like this story?
![]() |
UBAO WA MATANGAZO KATIKA SHULE YA SEKONDARI WASICHANA ST FRANCIS |
![]() |
MMOJA WA WAALIMU WA ST FRANCES AKITOA MAELEZO |
![]() |
MMOJA YA MAJENGO YA SHULE HIYO YANAYOTUMIKA KUTOLEA ELIMU |
Na David Nyembe,Mbeya
Ubora wa Mazingira katika shule ya Shule ya Sekondari ya
St.Francis ya Jijini Mbeya, Tanzania, wametajwa kuwa chachu ya mafanikio ya
shule hiyo.
Moja ya vitu muhimu vinavyo fanya shule hiyo kuwa bora ni pamoja
na suala la upatikanaji wa chakula bora cha kuwajenga wanafunzi pamoja na
upatikanaji wa vifaa muhimu vya kufundishia.
Hata hivyo Uongozi huo umedai kuwa ili
mwanafunzi aweze kufanya vizuri katika mitihani na kuendelea katika elimu ya
juu anapaswa kuzingatia mambo ya msingi ya: kimaadili, kuipenda shule na
kuwapenda na kuwaheshimu walimu na kuamini kuwa ni sehemu ya wazazi wao katika
malezi.
Akizungumza jijini mbeya Mkuu wa shule hiyo Sista Flossy Sequira
Amesema siri kubwa katika mafanikio ya shule hiyo ni kumtanguliza mungu kwanza
pamoja na kila mmoja katika shule hiyo kuanzia na uongozi hadi
walimu kutambua wajibu wao wa kazi.
Hata hivyo amedai kuwa mambo mengine ni
kuangalia lengo la msingi lililowafikisha shule, mpango mikakati ya kufikia
lengo ikiwemo na mbinu za kuondokana ama kutatua vikwazo vitakavyojitokeza
shuleni hapo .
.
K wa upande wake Mmoja wa walimu wa shule hiyo
Ndugu Erasto Batholomeo ambaye ni mwalimu wa Hisabati amesema kuwa endapo
wataona mwenzao yupo nyuma katika masomo wanamuunganisha na mwanafunzi
anayefanya vizuri katika darasa husika na kumpatia maswali hadi anafikia
kiwango cha daraja la A kama ilivyo lengo lao kwa wanafunzi wote, kwa mujibu wa
taratibu za uongozi wa shule.
Amesema sifa ya mafaniko mengine kwa
mwanafuzni wa shule hiyo kufanya vizuri ni kutokana na uwepo wa mazingira
mazuri ya kujisomea pamoja na upatikananji wa chakula bora ambacho
humjenga mwanafuzni kiulewa zaidi mara awapo darasani .
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SIRI YA UFAULU WA ST FRANCES MBEYA”
Post a Comment