Wednesday, February 26, 2014

JIJI LA MBEYA LAPATA MKANDARASI MPYA SOKO LA MWANJELWA


MWONEKANO WA SOKO JIPYA LA MWANJELWA JIJINI MBEYA

Na David Nyembe, Mbeya.
 
HALMASHAURI ya Jiji la Mbeya,  leo  limemkabidhi  Soko jipya la Kisasa la Mwanjelwa  mkandarasi mpya  kutoka Kampuni ya Nandhra  Engineering & Construction Company   baada ya mkandarasi wa awali   kuvunja mkataba.
 
Kuvunja kwa mkataba  huo, kumetokana na  Mkandarasi huyo  kutoka Kampuni ya Tanzania Bulding Works Limitted ya Jijini Dar es Salaam,  kushindwa kukamilisha ujenzi wa soko  hilo kwa wakati kwani  Julai 2012  soko hilo lilipaswa kukamilika na kukabidhiwa kwa uongozi wa halmashauri ya Jiji la Mbeya.
 
 
Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Mussa  Mapunda, amesema   mkandarasi huyo mpaya atatuumia shilingi bilioni 5.0 katika kukamilisha ujenzi wa soko hilo ambao mpaka sasa umetumia zaidi ya  shilingi Bilioni 11 kati ya Bilioni 13 .
 
Amesema, katika kiasi hicho cha fedha cha shilingi bilioni 13 kiasi kilichobakia ni shilingi Bilioni 1.8 hivyo kuilazimu halmashauri hiyo kukopa tena kiasi cha fedha cha  shilingi Bilioni 3.5 kutoka Benki ya CRDB kwa ajili ya kumalizia ujenzi  huo.
 
Akikabidhiwa ujenzi wa Soko hilo  Mkandarasi  Kulwant Singh aliwahahidi wakazi wa Jiji la mbeya na uongozi kwa ujumla kuwa atahakikisha kazi hiyo itakamilika katika kipindi walichoandikiana kwenye mkataba hivyo serikali kuondoa mashaka.
Ujenzi huo unadaiwa kusimama kwa  zaidi ya miezi  saba tangu Mkandarasi wa awali asitishe mkataba wake na kwamba ujenzi huo unatarajia kuanza  Aprili mwaka huu  na kukabidhi soko hilo Desemba mwaka huu
 
Soko la Mwanjelwa liliteketea kwa moto mwaka 2006 na kusababisha hasara ya mamilioni ya fedha kutoka kwa wafanyabiashara zaidi ya 2000 walionguliwa maduka yao.
Mwisho.

0 Responses to “JIJI LA MBEYA LAPATA MKANDARASI MPYA SOKO LA MWANJELWA”

Post a Comment

More to Read