Thursday, February 27, 2014
WANANCHI WA MBEYA WAELEZA HISIA ZAO BAADA YA MCHEZAJI WA MBEYA CITY KUITWA KWENYE KIKOSI CHA TAIFA
Do you like this story?
KIKOSI CHA MBEYA CITY |
![]() |
BAADHI YA MASHABIKI WA MBEYA CITY |
Na David Nyembe
Wakazi wa jiji la mbeya na vitogoji vyake wameeleza na kufuraishwa
kwao na hatua ya kocha mkuu wa timu ya taifa (Taifa Stars) kuchukua mmoja ya
wachezaji wa Mbeya City Fc Hassan Mwasapili ambayo inashiriki Ligi kuu Tanzania
Bara.
Wakizungumza jijini Mbeya wakazi hao wamesema hatua hiyo
inaleta chachu kwa vijana kuendelea kupenda mpira kwakuona ndio sehemu pekee ya
kujiajiri wenyewe na kujipatia kipato badala ya kusubiri kuajiriwa.
Mmoja wa wakazi hao Bi Silivia Tawete mkazi wa soko matola
amesema kuwa kwa muda mrefu Mpira ulikuwa haupendwi lkn kwa sasa ndio kimbilio
kwa vijana wengi.
Kwaupande wake msemaji wa timu ya Mbeya City Bw Fredy Jackson
ameonesha kufurahishwa na uteuzi huo huku akiamini kwamba umeleta hamasa kwa
wachezaji wengine wa Mbeya City na mashabiki wake kwani mchezaji huyo
hawakilishi Mbeya tu Bali ni taifa zima.
Hata hivyo amesema kuwa hatua hiyo itaendelea kuinua hali na
nguvu na kuwapa hamasa wachezaji hao kuendelea kufanya vyema katika timu yao
hatimaye waweze kufikia malengo yao.
Naye Mkazi wa eneo la Uhindini jijini mbeya Bwana Innocent
John amedai kuwa hatua ya kocha kushuka chini na kuchukua wachezaji kwenye timu
nyingine kunaonyesha wazi kuwa soka la Tanzania linaendelea kukua kwa kasi
kwani awali ilizoereka kuwa wachezaji shiriki kwenye timu ya Taifa ni Simba na
Yanga pekee hivyo hatua hiyo ni nzuri.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WANANCHI WA MBEYA WAELEZA HISIA ZAO BAADA YA MCHEZAJI WA MBEYA CITY KUITWA KWENYE KIKOSI CHA TAIFA”
Post a Comment