Tuesday, February 25, 2014
WATU WANAOSADIKIKA KUWA NI MAJAMBAZI WAFUNGA BARABARA MBEYA/NJOMBE WAPORA MALI NA KUJERUHI
Do you like this story?
![]() |
Kamanda wa mkoa mbeya Ahmed Msangi (Picha na Maktaba) |
Na David Nyembe ,Mbeya.
POLISI Mkoani Mbeya, inawashikilia watu 10 wanaosadikiwa ni
majambazi kwa tuhuma za kushusika na ufungaji wa barabara kuu ya
Mbeya/Njombe na kufanikiwa kupora mali za abiria waliokuwa wakisafiri na
kujeruhi watatu.
Kaimu Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Mbeya, Robert Mayala, amesema tukio hilo limetokea February 24 mwaka
huu majira ya saa saba za usiku katika Kijiji cha Machimbo Tarafa ya Rujewa
wilayani Mbarali.
Amesema,watu hao wakiwa na silaha za jadi, mapanga, marungu, mawe
na fimbo waliweka mawe makubwa na magogo kwenye barabara hiyo na kuteka baadhi
ya magari yaliyokuwa yakipita.
Amesema, baadhi ya abiria waliporwa fedha taslimu, simu za mkononi
na mikoba ambayo thamani na idadi bado haijafahamika huku abiria watatu wakijeruhiwa
kwa kupigwa sehemu mbalimbali za miili yao kwa kutumia silaha za jadi.
Mbali na kujeruhi na kuiba vitu mbalimbali pia wahalifu hawa wamefanya uharibifu katika baadhi ya magari kwa kuvunja vioo ikiwa ni pamoja na gari lenye namba za usajili T.867 ARX aina ya Toyota Noah lililokuwa likiendeshwa na dereva Ahmed Abdalah,” amesema Mayala.
Hata hivyo, amesema Askari waliokuwa doria kutoka Mkoa wa
Mbeya na Njombe walifanikiwa kufika kwa wakati kwenye eneo la tukio na kukuta magari yakiwemo yanayosafirishwa
kwenda nje ya nchi(IT) yakiwa yamesimamishwa na kwamba watu hao walipoona
gari la polisi walikimbilia vichakani na magari kuendelea na safari zake.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WATU WANAOSADIKIKA KUWA NI MAJAMBAZI WAFUNGA BARABARA MBEYA/NJOMBE WAPORA MALI NA KUJERUHI”
Post a Comment