Friday, February 28, 2014
SERIKALI YA NUNUA BUNDUKI BUNDUKI 500 ZA AK47 KUKABILI UJANGILI
Do you like this story?
![]() |
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII RAZARO NYALANDU |
![]() |
AK 47 |
Dar es salaam. Siku moja baada
ya Tanzania kutajwa na shirika la polisi la kimataifa (Interpol)kuwa kinara wa
biashara ya meno ya tembo Africa Mashariki, Serikali imelipia kodi na
kukabidhiwa bunduki 500 aina ya AK47 ili kukabiliana na ujangili katika hifadhi
na mapori ya akiba nchini
Waziri wa Maliasili na Utalii,
Lazaro Nyarandu alisema jana kuwa silaha hizo zilikuwa chini ya Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA), tangu November 2012 kutokana na kutolipiwa kodi
zitasambazwa Ngorongoro, selous, pamoja na hifashi za Taifa za Tanapa.
Kati ya shilaha hizo, 250 zitapelekwa kwa idara ya wanyamapori, 200
Tanapa na 50 Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro.
“Silaha hizi jumla y ash 427
milioni kuzinunua lakini zilikwama TRA kwa sababu ya kutolipiwa kodi na ushuru
mbali8mbali, hivyo wizara yangu leo inatoa sh 212 milion kwa ajili ya malipo
hayo” alisema Waziri Nyarandu.
Alisema silaha hizo
zimekombolewa ikiwa sehemu ya kutekeleza maazimio ya Bunge na ahadi ya serikali
kwa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maliasili ,Ardhi na Mazingira.
Akizungumzia sababu za
kuchelewa TRA, Nyarandu amesema kulikuwa na ubishi wa ama zilipaswa kulipiwa
kodi au la, lakini mamlaka hiyo ilifafanua kuwa h ayo ndiyo matakwa ya sheria,
hivyo akaamua kutoa fedha hizo.
Silaha hizo zimepatikana ikiwa
ni takribani wiki mbili tangu Raisi Jakaya Kikwete abanwe na vyombo vya habari vya kimataifa akitakiwa
kueleza mikakati iliyopo kupambana na ujangili ambao umeharibu sura ya Tanzania
nje ya nchi.
Itakumbukwa kuwa miezi miwili
iliyopita , Rais Jakaya Kikwete alilazimika kupangua Baraza la Mawaziri na
kuwatimua mawaziri wane kutokana na vitendo vya kinyama vilivyobainishwa na
kamati ya Bunge ya Maliasili na Mazingira wakati wa operesheni Tokomeza
Ujangili.
Majangili
papa 40
Akijibu maswali ya waandishi wa habari, Waziri
Nyarandu alisema majina ya majangili papa 40 ambayo Rais Kikwete alisema anayo,
‘yatabandikwa’ hivi karibuni .
Amesema, Serikali inawafahamu majangili hao kwa
udani, wanapokunywa chai,wanapotembelea na shughuli zao za kila siku.
Amesema majina yao si siri kwani tayari
wameshafunguliwa mashtaka na wapo chini ya mfumo wa mahakama na wamekamatwa na
vidhibiti.
Hivi karibuni, Rais Kikwete alihojiwa na shirika
la utangazaji la Uingereza( BBC),
alisema serikali ina majina 40 ya majangili papa na mkuu wao yuko
Arusha.
Selous
Yaimarishwa
Katika
hatua nyingine, waziri Nyarandu alitangaza kuzipandisha hadhi kand nane
zalizopo katika pori la Akiba la Selous, ili ziweze kujitegemea kiutendani kwa
kuweka mkuu wa kila kanda.
Alisema pori hilo lina ukubwa unaokaribia
hifadhi zote za Taifa chini ya Tanapa ,
jambo linalolifanya kuwa kubwa kimenejiment na kuuendeshaji.
Pori la selous lina kilomita za maraba 55,000
wkati mapori yote nchini kwa ukubwa wake ni kilomita za mraba 57,000 .
Katika kuweka mazingira ya uangalizi wa kina ya
kupambana na ujangili, aliiagiza idara ya Wanyamapori kukamilisha mchakato wa
kufungua akaunti maalumu za benki kwa kila kanda ili kuwawezesha wakuu wa kand kutekeleza
majukumu yao kwa ufanisi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI YA NUNUA BUNDUKI BUNDUKI 500 ZA AK47 KUKABILI UJANGILI”
Post a Comment