Friday, February 28, 2014
BANDARI YA DAR ES SALAAM KUANZA KUTOA HUDUMA MASAA 24
Do you like this story?
![]() |
BANDARI YA DAR ES SALAAM |
Dar es salaam. Mamlaka ya
Bandari Tanzania (TPA) ikishirikiana na wadau wake kuanzia kesho wanatarajia
kuanza kutoa huduma kwa saa 24, siku saba katika wiki, mwaka mzima bila
kupumzika.
Ofisa Uhusiano wa TPA,
Janeth Zurngi alisema uamuzi huo ambao unakusudia kuongeza ufanisi wa bandari
hiyo, umefikiwa baada ya wadau mbalimbali kutia saini mikataba ya utekelezaji
kazi hiyo.
Zurangi Amesema ingawa
kulikuwapo mabishano kuhusu vipengele kadhaa ndani ya mkataba huo, wadau wote
walikubali kuanza kutoa huduma kila siku kwa saa 24 kuanzia Machi Mosi.
“Mwezi ujao utaratibu huo utaanza na tunatarajia
utakuwa na mafanikio makubwa. Hivi sasa mteja anaweza kuchelwa kuchukua mzigo
kwa sababu baadhi ya wadau hawajasaini vibali husika”, alisema.
Oktoba 14 mwaka jana ,
Waziri wa Uchukuzi, DK Harrison Mwakyembe aliwataka wadau wengine wanaofanya
kazi TPA kuanzisha utaratibu wa kufanya kazi kila siku, kwa kile alichoeleza kutofanya hivyo kunakwamisha
kasi ya uondoaaji mizigo bandarini.
DK Mwakyembe alinukuliwa akisema:
“Bandari wanafanya kazi saa 24 kwa siku saba za wiki bila kupumzika,
lakiniwenzetu wa TRA wao sikukuu na siku za mwisho wa juma wanalala hali hii
itaturudisha nyuma kimapato
” Baadhi ya wadu walisaini mkataba huo ni Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA), Chama cha Wakala wa Forodha na Uondoshaji Shehena
Tanzania (Taffa)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BANDARI YA DAR ES SALAAM KUANZA KUTOA HUDUMA MASAA 24 ”
Post a Comment