Tuesday, April 15, 2014
HIZI HAPA SABABU ZINAZOWAFANYA MBEYA CITY FC KUWA BORA MSIMU HUU.
Do you like this story?
MBEYA CITY fc
ni klabu ya kwanza kuipatia Azam fc ubingwa wake wa kwanza tangu ianze
kushiriki michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2008/2009.
Ardhi ya
Mbeya imekuwa ya kwanza kwa Azam fc kutwaa ubingwa ndani yake.
Azam fc
imekuwa klabu ya kwanza kuwafunga Mbeya City msimu huu katika uwanja wao wa
nyumbani wa kumbukumbu ya Sokoine.
Kocha
Mcameroon, Joseph Marius Omog amekuwa kocha wa kwanza kuwapatia mafanikio ya
ubingwa wa ligi kuu Azam fc.
Rekodi nyingi
sana zimewekwa kwa Azam fc msimu huu, lakini yote hii inatokana na ubingwa huo
kuwa wa kwanza kwao.
Msimu wa
mwaka huu umekuwa na ushindani mkubwa mno hasa katika nafasi ya ubingwa.
Klabu mbili
kongwe za Simba na Yanga zimekumbana na changamoto kubwa kutoka kwa Azam fc na
Mbeya City katika nafasi nne za juu.
Mpaka sasa
kimeeleweka ambapo Yanga pekee wameweza kushika nafasi ya pili, wakati Simba
wakitupwa nafasi ya nne.
Imekuwa kazi
ngumu kwa wafalme hawa wa soka la Tanzania kutoka mwaka 2000 kuachia ubingwa
zaidi ya kupokezana kama mbio za vijiti.
Wana TamTam
Mtibwa Sugar walibeba `ndoo` mwaka 1999 na 2000, baada ya hapo Simba na Yanga
walikuwa wanatawala, lakini mwaka huu 2014 wamepinduliwa rasmi kwa Azam fc
kutwaa taji.
Cheche
zinawaka zaidi kwa Simba kwasababu kwa misimu miwili mfululizo wanakosa
michuano ya kimataifa.
Angalau Yanga
mwaka huu walishiriki ligi ya mabingwa na kuonesha upinzani mkubwa, na mwakani
wataiwakilisha Tanzania katika michuano ya kombe la shirikisho.
Kwa upande wa
Simba imekuwa pigo kwao kwasababu mashabiki wake walizoea kuona timu yao
inawakilisha bendara ya Tanzania kimataifa.
Azam fc
wamestahili kutwaa ubingwa kwasababu ya uwekezaji mkubwa waliouweka katika
kikosi chao kuanzia vifaa vya mazoezi na mazingira ya kambi kwa wachezaji.
Ingekuwa
fedhea kwao kukosa ubingwa, kwasababu hawakustahili kushika nafasi ya pili
ambayo wameshaishika sana misimu ya nyuma.
Matokeo
mazuri kwao ilikuwa ni ubingwa tu na ndio maana waliweka mikakati mikubwa ya
kufanya vizuri na katika mechi 25 walizocheza hawajapoteza mechi yoyote
Ukirejea kwa
Mbeya City fc, hii ni klabu pekee iliyopanda ligi kuu msimu huu na kuonesha
ushindani mkubwa kutoka mwanzo wa ligi mpaka sasa ligi inaelekea ukiongoni.
Wenzao
Ashanti hatima yao imebakia mikononi kwa kocha wa Prisons, David Mwamwaja mnamo
aprili 19 mwaka huu.
Kama watatoa
sare mechi hiyo watashuka daraja, na matokoe pekee yatakayowasaidia ni kushinda
tu.
Rhino Rnagers
wao wameshashuka daraja mpaka sasa.
Kwa mazingira
hayo, Mbeya City imekuwa timu bora zaidi msimu huu ukiangalia kigezo cha ugeni
wa ligi kuu.
Huwezi
kuwafananisha Mbeya City na Azam fc, Yanga, Simba, Mtibwa, Kagera Sugar,
Coastal Union kwa kigezo cha ukongwe.
Wao ni wageni
sana kwani ndio kwanza msimu wao wa kwanza.
Wachezaji
wengi wa Mbeya City ni wageni na hawana majina kabisa katika soka la Tanzania.
Mpaka sasa
wagonga nyundo hawa wa Mbeya wamecheza mechi 25 na kushinda mechi 12, sare
mechi 10 na kufungwa mechi 3. Kwa matokeo hayo wamefikisha pointi 46 katika
nafasi ya nne.
Hata hivyo
safu yao ya ushambuliani imeweza kufunga mabao 32, huku safu ya ulinzi
ikiruhusu kufungwa mabao 20.
Yanga
waliwafunga Mbeya city bao 1-0 katika uwanja wa Taifa na kule Mbeya mzunguko wa
kwanza walitoka sare ya bao 1-1 katika dimba la Sokoine.
Coastal Union
katika mechi ya mzunguko wa kwanza walitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Mbeya City
uwanja wa sokoine, lakini mechi ya mzunguko wa pili Mkwakwani, wagosi
wakashinda mabao 2-o.
Simba
waliambulia pointi moja moja kwa mechi zote mbili ambapo Mbeya walitoka sare ya
1-1 na Dar es salaam walitoka sare ya 2-2.
Azam fc
katika mechi ya kwanza chamazi, walilazimisha sare ya mabao 3-3 na Mbeya
wakashinda 2-1 na kutwaa kombe huko huko.
Kwa mazingira
hayo, Yanga, Coastal na Azam fc ni timu pekee zilizoweza kuifunga Mbeya City.
Nini kimekuwa
nyuma ya Mbeya City mpaka wanakuw ana upinzani mkubwa kiasi hicho?
Baadhi ya
sababu ambazo zinawapa nguvu wagonga nyundo hawa wa Mbeya zaweza kuwa ni;
Mosi; falsafa
ya kocha mkuu, Juma Mwambusi na msaidizi wake, Maka Mwalwisyi.
Makocha hawa
wanaamini katika soka la vijana na kuwapa nafasi ya kucheza kwa mechi yoyote
ile.
Mara nyingi
Mwambusi anaeleza kuwa mchezaji yoyote unayemuona bora duniani alipewa nafasi
ya kucheza na akafanikiwa kupata uzoefu mkubwa na kung`ara.
Kwa mantiki
hiyo, huwa anawapa vijana wake nafasi na kukwepa kuonesha kuwa anawategemea
wachezaji fulani.
Mwambusi
amekuwa akichagua timu yake kwa kuangalia ufiti wa mchezaji kwa mechi fulani na
anaweza kuwabadilisha anavyotaka.
Katika kikosi
chake hakuna mchezaji tegemeo, na ndio maana leo hii unaweza kumuona Mwegane
Yeya yuko benchi, lakini Jeremiah Peter yupo uwanjani na anafanya kazi
kubwa.
Ukiona Paul
Nonga unaweza kuogoapa kuwa hawatafunga, lakini unashangaa kumuona Peter
Mapunda amevaa jezi ya zambarau na kuonesha soka zuri mno.
Kwa mzingira
haya, wachezaji wanajiamini na kuamini kuwa watapangwa wakati wowote, cha
msingi wajitume katika mazoezi.
Kwa hili
Mwambusi ameweza kuwaweka pamoja wachezaji wake na kuooneana wivu kwenye mechi.
Pili;
kujielewa kwa wachezaji wa Mbeya City fc. Ni ngumu sana kugundua kuwa wachezaji
wa klabu hii wapo katika dhiki fulani.
Lakini
taarifa za kuaminika kutoka ndani ya timu hii ni kuwa kuna wakati wachezaji
wanacheleweshewa mishahara yao na posho.
Wakati wote
wamekuwa wavumilivu sana na hii inatokana na makocha wao kuwajenga katika
mazingira ya kuamini kuwa Mbeya City wanapita na safari yao ni kwenda
kimataifa.
Wanapenda
kufanya kazi yao na ni wazalendo wakubwa mno, huku wakiamini kuwa ipi siku
watauzika.
Ukiwa na
wachezaji wenye malengo ya kufanya kazi kwanza na kusubiri mafanikio baadaye
basi watakusaidia kama ilivyo kwa Juma Mwambusi.
Tatu; nidhamu
kubwa kwa wachezaji. Vijana wa Mbeya City fc wana nidhamu nzuri uwanjani na nje
ya uwanja.
Wamejengwa
katika misingi ya kuheshimu miiko ya mpira, hivyo ni ngumu kuwaona wakifanya
makosa ya kujirudia rudia au kufanya fujo uwanjani.
Kwa mara ya
kwanza walionekana kuwa na hasira katika mechi iliyopita dhidi ya Azam fc na
sababu kubwa ilikuwa ni presha ya mchezo wenyewe.
Lakini kwa
takribani msimu mzima wamekuw a na nidhamu nzuri ikiwepo nidhamu ya uwanjani.
Nne;
kufanikiwa kucheza kitimu; Mwambusi amefanikiwa kwa hili kama makocha wengi
duniani wapendavyo.
Kuwa na timu
inayocheza kitimu bila kutegemea matokoe kwa wachezaji fulani ni faida kubwa
mno.
Hata timu
kubwa duniani kuna wakati zinajenga matokeo yake kupitia mchezaji mmoja.
Mfano kwa
muda mrefu Lionel Messi amekuwa mwamuzi wa matokoe kwa FC Barcelona pamoja na
Cristiano Ronaldo kwa Real Madrid.
Wachezaji
hawa wanapokabwa ile `ngado kwa ngado` basi timu nzima inapwaya.
Lakini kwa
kocha Mwambusi imekuwa ni tofauti. Timu yake imekuwa ikicheza kitimu na kila
anapokosekana mchezaji mmoja basi hakuna shida.
Tano;
Wachezaji kuwa na nguvu za kucheza kwa dakika zote. Wanandinga wa Mbeya City
wana uwezo wa kucheza kwa dakika zote na kuhimili presha ya mchezo.
Hawaishiwi na
pumzi ndani ya dakika 90. Haya ni matunda ya maandalizi yao ya muda mrefu.
Wamekuwa
hawatabiriki wanapokuwa uwanjani. Kwa muda wote wanacheza kwa kasi nzuri na
kuilinda mpaka mwisho wa mchezo.
Pia hili
limewabeba sana tofauti na timu nyingine zinazokata pumzi katika dakika fulani.
Sita;
Mashabiki wengi kuwepo nyuma yao. Kwa msimu mzima mashabiki wa soka mkoani
Mbeya wamekuwa nyuma ya klabu yao na wanaweza kusafiri kwenda mikoani
kuishangilia timu yao.
Wameleta
utamaduni mpya kwa timu za Tanzania kwani ni kawaida kuikuta Simba akicheza na
Oljoro lakini mashabiki wa Arusha wanaishangilia Simba badala ya timu yao.
Kwa Mbeya
imekuwa ni tafouti kabisa hata Simba na Yanga zimepoteza mashabiki wengi.
Wachezaji
wanafurahi kuona mashabiki wengi wapo nyuma yao, hivyo kucheza kwa kujituma ili
kuwalipa fadhila.
Mashabiki ni
wachezaji wa kumi na mbili, hivyo Mbeya wamefanikiwa kwa hili na ndio sababu ya
timu yao kufanya vizuri msimu huu.
Hizi si
sababu pekee zilizowafanya Mbeya City fc kufika hapo walipo, bali zipo nyingine
nyingi ambazo nitazieleza baadaye.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “HIZI HAPA SABABU ZINAZOWAFANYA MBEYA CITY FC KUWA BORA MSIMU HUU.”
Post a Comment