Tuesday, April 15, 2014
YANGA WAKIJIANDAA KUMALIZA HASIRA KWA SIMBA, UCHAGUZI JUNI 15 MWAKA HUU!!.
Do you like this story?
YANGA
wanajiandaa kufuta machungu ya kupoteza ubingwa wao msimu huu kwa wana
Lambalamba Azam fc kwa kuhakikisha wanaibuka kidedea katika mchezo wa jumamosi
(aprili 19) mwaka huu dhidi ya mahasimu wao wa jadi, wekundu wa Msimbazi Simba.
Yanga
wapo mjini Moshi, mkoani Kilimanajaro na leo hii wanatarajia
kucheza mechi ya kirafiki na moja ya timu ya mkoani humo.
Charles
Boniface Mkwasa `Master`, kocha msaidizi wa Yanga amesema malengo yao ni
kuhakikisha wanawafunga Simba hata kama wameshapoteza ubingwa.
Yanga walioambula
nafasi ya pili msimu huu na kuwa wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya
kombe la shirikisho mwakani wataingia uwanjani kucheza na Simba yenye mwendo wa
kusuasua msimu huu.
Hata hivyo
nao Simba wamekuwa wakitamba kuwa mechi yao na Yanga watapambana kwa nguvu zote
ili kuwaumiza Yanga mara mbili .
Endapo Yanga
watafungwa mechi hiyo, basi watakuwa na maumivu ya kupoteza ubingwa na
kufungwa na mahasimu wao Simba sc.
Mechi ya
Yanga na Simba huvuta hisia za mashabiki wa soka nchini, na hivi sasa kila kona
joto limeanza kupanda.
Huwa ni raha
sana kwa timu moja kuifunga timu nyingine baina ya klabu hizi kongwe nchini.
Mechi
iliyopita ya ligi kuu bara Yanga walishinda mabao 2-1 dhidi ya JKT Oljoro
katika dimba la Shk. Amri Abeid jijini Arusha na kufikisha pointi 55 katika
nafasi ya pili, wakati Simba walipoteza kwa bao 1-0 dhidi ya Ashanti
ndani ya uwanja wa Taifa na kubakia na pointi zao 37 katika nafasi ya
nne.
Wakati timu hizi zikiwa katika
maandalizi ya mechi hiyo, taarifa kutoka ndani ya klabu ya Yanga zinaeleza kuwa
Kikao cha Kamati ya Utendaji kilichokaa tarehe 10 Aprili 2014 Makao Makuu
ya klabu kilikubaliana kuwa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa YANGA SC utafanyika
tarehe 15 Juni 2014.
Taarifa za taratibu za Uchaguzi
zitatangazwa hapo baadaye na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Mh Alex Mgogolwa.
Hii itakuwa fursa kwa wanachama wa
Yanga kuomba nafasi mbalimbali klabuni hapo.
Ikumbukwe kuwa mwenyekiti wa sasa wa
Yanga, Yusuf Manji alishawahi kutangaza siku za nyuma kuwa hatagombea tena
nafasi hiyo.
Tamko la Manji liliwagusa wana Yanga
wengi wenye mapenzi na kiongozi huyo aliyeisaidia Yanga kufika hapo ilipo.
Manji katika muda wake wa udhamini na
Uongozi, amekuwa akiifanyia timu mambo makubwa ikiwemo usajili wa wachezaji
ghali na kuweza kuweka kambi nje ya nchi hususani barani Ulaya.
Tusubiri kama nia yake ya kutogombea
ipo palepale au atabadili maamuzi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “YANGA WAKIJIANDAA KUMALIZA HASIRA KWA SIMBA, UCHAGUZI JUNI 15 MWAKA HUU!!.”
Post a Comment