Tuesday, April 15, 2014
MILIONI 34 ZAPATIKANA MECHI YA AZAM FC NA MBEYA CITY FC.
Do you like this story?
JUMLA
ya shilingi milioni 34,070,000 zimepatikana katika mechi ya Mbeya City na
Azam ya Jijini Dare es salaam iliyochezwa April 13 mwaka huu katika
uwanja wa kumbukumbu wa Sokoine huku timu ya Azam ikiondoka na Ushindi wa
goli 2-1.
Akisoma
mapato hayo Katibu wa chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA)
Selemani Harubu , amesema kati mapato hayo shilingi milioni 7,628,074.99
zimeenda kwa kila timu.
Amesema,
gharama ya Vat ni shilingi milioni 5,197.118.64 tiketi shilingi
3,015,000 gharama ya mchezo 2,327,209,305.32 huku kamati ya ligi
ikiondoka na shilingi 2,327,209.322.
Amesema,
TFF imepata shilingi 1,163,604.66 na MREFA ikiondoka na
shilingi 905,025,84 na uwanja ukipata shilingi 3,878,682.20.
Aidha
katika Mchezo baadhi ya wadau mbalimbali wa mpira jijini mbeya wamedai kuwa
ushindi huo wa Azam hakuwa sawa kwa madai kuwa mwamuzi wa mchezo huo Nathan
Lazaro kutoka Kilimanjalo kuwa aliipa ushindi Azam kwa goli lisilo halali .
Aidha
kufuatia matokeo hayo Azam wamejitawaza kuwa mabingwa wapya ligi kuu vodacom
Tanzania Bara kwa kufikisha Pointi 59 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote
huku ikibakiwa na mchezo mmoja mkononi .
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MILIONI 34 ZAPATIKANA MECHI YA AZAM FC NA MBEYA CITY FC.”
Post a Comment