Wednesday, April 2, 2014
KESI YA ZITTO YAZIDI KUPIGWA KALENDA.
Do you like this story?
Dar es salaam kesi ya
aliyekuwa naibu katibu mkuu wa chadema zitto kabwe dhidi ya chama chake
imepigwa kalenda hadi mei 29 2014 .
Kesi hiyo ilipangwa
kutajwa jana katika mahakama kuu kanda ya dare s salam jaji john utamwa anayeisikiliza lakini iliahirishwa na msajili wa wilaya ya wa mahakama kuu kanda ya dar es salaam amir msumi.
Akiahirisha kesi hiyo
msumi alisema jaji utamwa hakuweza
kufika jana kwa sababu anaumwa na akapanga kesi hiyo itajwe mahakamani
hapo tarehe hiyo.
Hii ni mar aya pili kwa
kesi hiyo kuahirishwa na wasajili
kutokana na sababu za ugonjwa wa jaji
utamwa mara ya kwanza iliahirishwa
na msajili wiliam mtaki Februari 13 2014
Zitto ambaye pia ni mbunge
wa kigoma kaskazini alifungua kesi h iyo dhidi ya bodi ya wadhamini wa chadema
akiomba mahakama hiyo ikizuie chama kujadili uanachama wake
hadi rufaa anayokusudia kuikata baraza kuu la chama kupinga kuvuliwa
nyadhifa itakaposikilizwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KESI YA ZITTO YAZIDI KUPIGWA KALENDA.”
Post a Comment