Wednesday, April 16, 2014
POLISI YATANGAZA DAU MILIONI 10/- KUMNASA MLIPUAJI BOMU ARUSHA.
Do you like this story?
Aidha polisi imetangaza zawadi ya Sh milioni
10 kwa mtu atakayetoa taarifa juu ya wanaohusika katika kulipua
mabomu, ikiwa ni pamoja na waliolipua baa ya Arusha Night Park ya jijini
hapa.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini
(DCI), Isaya Mngulu alikuwa akizungumza na waandishi wa habari jana kuhusu
tukio hilo la Jumapili, saa 1:30 usiku eneo la Mianzini kwenye baa hiyo
inayomilikiwa na Joseph Kalugendo.
Alisema wataalamu wa mabomu waligundua bomu
lingine saa 6:00 usiku kwenye baa iliyo karibu na baa hiyo likiwa ndani ya begi
dogo.Uchunguzi wa awali umebaini bomu hilo ni kifaa cha mlipuko wa kutengenezwa
kienyeji.
Alisisitiza hadi sasa, hawajakamata mtu yeyote
kuhusu tukio hilo huku uchunguzi ukiwa unaendelea.
Alisema majeruhi waliobaki wadini ni wanane
na wengine wameruhusiwa. Walio wodini ni Evance Maleko, Evarist Richard, Petro
James, Christian Zakaria, Pius Shayo, Antelus Ishengoma, Sudi Ramadhani
na Mariam Hans aliyepo hospitali ya Selian.
.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “POLISI YATANGAZA DAU MILIONI 10/- KUMNASA MLIPUAJI BOMU ARUSHA.”
Post a Comment