Tuesday, April 15, 2014
PRISON WAKIRI KUWA PETER MICHAEL AMECHANGIA TIMU KUWA PABAYA.
Do you like this story?
Licha ya
kufunga mabao matano katika mzunguko wa pili wa ligi kuu, Tanzania,mshambuliaji
wa timu ya soka ya Tanzania Prisons ametupiwa lawama kuwa kupoteza kwake nafasi
za kufunga magoli kumechangia timu hiyo kuwa katika hatari ya
” Peter ni
mchezaji wetu, ni mfungaji wa kutegemewa katika timu lakini hatoi mchango wa
kutosha. Anapoteza sana nafasi, kitu ambacho kimetugharimu katika michezo minne
iliyopita”.
Kwa mujibu
wa chanzo chetu cha habari kutoka ndani kabisa ya timu hiyo, Peter mwenye mabao
tisa msimu huu ameambiwa anatakiwa kuongeza umakini uwanjani ili kuinusuru timu
yake isishuke daraja.
” Mwalimu
ameliona hilo na kumtaka apigane kuisaidia timu. Kazi yake ni kufunga magoli
kitu ambacho ana uwezo nacho, ameambiwa kuongeza umakini na kutumia vizuri
nafasi anazopata.
Ligi
imekuwa ngumu lakini ni uzembe wetu wenyewe tuliofanya katika michezo ya
hivi karibuni iliyopelea hali hii”.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “PRISON WAKIRI KUWA PETER MICHAEL AMECHANGIA TIMU KUWA PABAYA.”
Post a Comment