Monday, April 14, 2014
UPDATES:MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZUNGUMZIA TUKIO LA BOMU KULIPUKA KWENYE BAA USIKU APRILI 13, 2014.
Do you like this story?
Usiku wa April 13 2014 kwenye baa
iitwayo ‘Arusha night park’ iliyopo Mianzini Arusha ambayo siku zote ni
miongoni mwa sehemu zinazokua na mkusanyiko wa watu wengi kuanzia jioni,
limerushwa bomu wakati watu mbalimbali wakitazama mpira.
Blog hii
imepata nafasi ya kuongea na mkuu wa mkoa wa Arusha ambae ni kiongozi wa Kamati
ya ulinzi na usalama ya mkoa ambae amethibitisha kwamba ni watu 15 wamejeruhiwa
kwenye mlipuko huo.
Anasema wote
wamepelekwa hospitali ambapo uchunguzi wa awali umeonyesha bomu hilo ni la
kutengenezwa kwa mkono na mpaka sasa hajajulikana alietekeleza shambulio hilo.
Kwenye sentensi nyingine pia amesema
hakuna aliepoteza maisha kwenye shambulio hilo ambalo uchunguzi wa awali
umeshatoka, ila baadae itatoka taarifa rasmi pale uchunguzi kamili
utakapokamilika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “UPDATES:MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZUNGUMZIA TUKIO LA BOMU KULIPUKA KWENYE BAA USIKU APRILI 13, 2014.”
Post a Comment