Saturday, April 12, 2014

WANANCHI WAKOSA HUDUMA ZA AFYA KISA MUUGUZI KWENDA LIKIZO.


Mkuu wa Wilaya ya Chunya Bw Deodatus kinawilo


Hii ndio Zahanati ya kijiji cha gua kata ya gua ambayo umefungwa takribani mwezi mmoja.


WANANCHI wa Kata ya Gua iliyopo Wilayani Chunya, Mkoani Mbeya, wameilalamikia serikali kwa kushindwa kupeleka watumishi kwenye  Zahanati ya afya hali iliyopeleka kufungwa kwa jengo hilo na wao kukosa huduma.

Zahanati hiyo imefungwa kwa zaidi ya mwezi mmoja kwa kile kinachosemekana mkunga aliyekuwepo kwenda likizo ya mapumziko.

Wakizungumza na Fahari news Blog wakazi wa Kijiji cha Gua Kata ya Gua, walisema  huduma kwenye Zahanati hiyo ilianza kusuasua  kuanzia mwezi January mwaka huu na ulipofika mwezi February ndipo waliposhangaa kuona jengo hilo limefungwa.
“Kipindi cha nyuma  huduma ilikuwa ikitolewa kwa kusuasua, lakini  hivi karibuni ndio tumeshangaa kukuta jengo hili likiwa limefungwa na tulipofuatilia  kwenye uongozi wa serikali ya kijiji tumeambiwa kuwa muuguzi aliyekuwepo ameenda mapumziko,”alisema Krispin Mikael mkazi wa Gua.

Amesema, awali  Zahanati  hiyo ilikuwa na mganga aliyetajwa kwa jina moja la Semwenza ambaye alistaafu na kijiji kukaa zaidi ya miaka miwili bila ya mganga  hivyo kuendeshwa na mkunga tu.

Amesema,  tatizo kubwa ni pale mkunga huyo anapopatwa na matatizo pamoja na kuchukua likizo ya mapumziko hivyo jengo hilo la Zahanati hufungwa na kumsubili mpaka siku atakapo rejea ofisini.

Amesema, katika kipindi chote  hicho   wagonjwa  huendelea kuteseka kwa kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta huduma na wengine huishia kwa waganga wa kienyeji.

Amesema,  baadhi ya wagonjwa hukimbilia  kwa waganga wakienyeji kutibiwa  ambao wengi wao hutumia ramli za uchonganishi na kusababisha migogoro isiyokuwa na ulazima ndani ya jamii.

Aidha, jitihada za  kumtafuta Mwenyekiti wa Kijiji hicho kwa nia ya kupata maelezo ya jambo hilo ziligonga mwamba baada ya kuelezwa kuwa kiongozi huyo alikuwa amesafiri kikazi.
Fahari News ilifanikiwa kuzungumza na Mkurugenzi wa

Halmashauri ya Chunya Sophia Kumbuli ambaye  aliahidi kulifanyia kazi tatizo hilo ikiwa ni pamoja na kufika kwenye eneo la tukio.

0 Responses to “WANANCHI WAKOSA HUDUMA ZA AFYA KISA MUUGUZI KWENDA LIKIZO.”

Post a Comment

More to Read