Thursday, June 19, 2014

BASI LA NEW FORCE LAUA WIWILI MBEYA.











Mkuu wa mkoa wa mbeya Abasi Kandoro akipewa maelezo na polisi wa usalama barabarani



Watu wawili Watembea kwa miguu wawili waliotambulika kwa majina ya  Theresia Hiingi (65)  Mary Kizito (26) wote wakazi wa igurusi wamefariki dunia baada ya kugongwa na basi la kampuni ya usafirishaji – new force lenye namba za usajili t. 952 cgu aina ya scania lililokuwa likiendeshwa na yahaya abdalah (39) mkazi wa dsm.

Tukio hilo limetokea mnamo tarehe 18.06.2014 majira ya saa 18:00 jioni katika kijiji cha igurusi, kata ya igurusi,  barabara kuu ya mbeya/njombe, wilaya ya mbarali, mkoa wa mbeya..

Inadaiwa kuwa basi hilo lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea mbeya mjini liligonga gari t. 954 amh aina ya  fuso lililokuwa likiendeshwa na dereva tupa anyosisye (32) mkazi wa kiwira –tukuyu, kisha kuacha njia na kuwagonga watembea.

Aidha katika ajali hiyo watu wengine wanne walijeruhiwa kati yao abiria mwanaume mmoja na wanawake watatu watembea kwa miguu wote wamelazwa katika hospitali ya misheni chimala.

Pia miili ya marehemu imehifadhiwa hospitalini hapo. Chanzo cha ajali ni mwendo kasi wa dereva wa basi, ambaye amekimbia mara baada ya ajali na juhudi za kumtafuta zinaendelea.

Kufuatia hali hiyo Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Ahmed Msangi anatoa wito kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto hasa kwa kuzingatia alama na sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoepukika.

Aidha anatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za mahali alipo mtuhumiwa wa tukio hili azitoe katika mamlaka husika ili akamatwe na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake

0 Responses to “BASI LA NEW FORCE LAUA WIWILI MBEYA.”

Post a Comment

More to Read