Tuesday, June 10, 2014
CHUI WAZUA MTAFARUKU BAADA YA KUVAMIA KIJIJI MOSHI VIJIJINI.
Do you like this story?
WAKAZI wa kijiji cha Okeseni
Chini, Wilaya ya Moshi Vijijini, mkoani Kilimanjaro, wanalala mapema
wakihofia kushambuliwa na kundi la wanyama aina ya Chui lililovamia kijiji
hicho.
Akizungumza kwa njia ya simu
jana, mmoja wa wakazi hao, Pamfill Shayo, alisema hivi sasa wanakijiji hao
wanaingia ndani saa 12 jioni na kulala wakiogopa kushambuliwa na chui hao ambao
tayari wameshaua mifugo ipatayo 25.
Alisema kundi hilo la Chui limekuwa
likirandaranda katika vichaka vilivyoko karibu na kijiji hicho na kila
giza linapoingia wanajitokeza, hali inayotishia usalama wa maisha yao.
“Hawa Chui hadi sasa wameua mbuzi,
mbwa, paka na kuku. Hali inatisha uanajua mnyama huyu alivyo na vurugu wakati
mwingine wanavamia kundi la mifugo na kuiua,”alisema Shayo.
Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Melkadeke
Mushi, alikiri kijiji hicho kuvamiwa na wanyama hao.
Hata hivyo, alisema taarifa
zimefikishwa kwenye Idara ya Wanyamapori, hivi sasa wanasubiriwa ili
kuwarudisha katika maeneo ya hifadhi ya taifa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “CHUI WAZUA MTAFARUKU BAADA YA KUVAMIA KIJIJI MOSHI VIJIJINI.”
Post a Comment