Tuesday, June 10, 2014
MSICHANA WA KAZI ALIYECHOMWA NA PASI NA KUTESWA NA BOSI WAKE KWA MIAKA 3 AKABIDHIWA KWA WANAHARAKATI
Do you like this story?
Hatimaye Yusta Lucas (20), binti aliyekuwa akiteswa kwa kuchomwa pasi na kung’atwa na mwajiri wake, Amina Maige ameruhusiwa kutoka Hospitali ya Mwananyamala alikokuwa amelazwa na kukabidhiwa kwa wanaharakati wa Taasisi ya Jipange.
Hatua hiyo
ilifikiwa baada ya maridhiano kati ya Ustawi wa Jamii, mama mzazi wa Yusta,
Modesta Simon, Kamati ya Ulinzi na Usalama Kata ya Makumbusho na Jipange ambao
ndiyo iliyofanikisha kumwokoa binti huyo.
Akizungumza
jana, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Makumbusho, Husna Nondo alisema baada ya
kutafakari kwa kina juu ya usalama na urahisi wa kupatikana pale
atakapohitajika, wamekubaliana binti huyo akae kwa muda kwa mmoja wa
wanakikundi kutoka taasisi hiyo.
“Tumeafikiana
Yusta aendelee kubaki mikononi mwa wanaharakati ili iwe rahisi kupatikana
atakapohitajika mahakamani, maana yeye ndiye shahidi wa kwanza. Mama na mjomba
wake waliotoka Tabora wataendelea kukaa Upanga walikofikia,” alisema Nondo.
Ofisa
Ustawi wa Jamii wa Hospitali ya Mwananyamala, Rose Temu alisema wamemkabidhi
Yusta kwa Jipange kwa maandishi na wanaamini yuko katika mikono salama kwa sababu
taasisi hiyo ndiyo iliyokuwa mstari wa mbele kumuokoa.
“Wakati
akisubiri kesi yake, tumekubaliana awe chini ya Jipange tumeona asiendelee
kukaa wodini kwan anaweza kupata ugonjwa mwingine, uamuzi ambao hata mama yake
ameuridhia.”
Mwenyekiti
wa Jipange, Janet Mawinza alisema wamekubali kumpokea Yusta kwa ajili ya
usalama wake lakini akasema hataeleza ni wapi atakuwa anaishi kwa kipindi
atakachokuwa akisubiri kesi.
“Sisi
tumempokea kama kikundi na tunachoomba ni vyombo vinavyohusika na suala hili
kuhakikisha vinashughulikia suala lake kwa wakati ili huyu binti aungane na
familia yake Tabora,” alisema.
Mama wa
binti huyo alisema anaamini binti yake yuko katika mikono salama. “Hawa
Jipange ndiyo walikuwa naye tangu siku ya kwanza na sioni kama kuna tatizo wao
kuendelea kuwa naye.”
Kwa siku
tano, Yusta alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Mwananyamala kuuguza majeraha
yanayodaiwa kusababishwa na kung’atwa na kuchomwa na pasi na Maige ambaye
alikuwa mwajiri wake huko Mwananyamala Kwa Manjunju kwa muda wa miaka mitatu.
Mtuhumiwa
anashikiliwa na Polisi katika Kituo cha Oysterbay na wakati wowote atafikishwa
mahakamani upelelezi utakapokamilika.
Credit: Mwananchi
Credit: Mwananchi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MSICHANA WA KAZI ALIYECHOMWA NA PASI NA KUTESWA NA BOSI WAKE KWA MIAKA 3 AKABIDHIWA KWA WANAHARAKATI ”
Post a Comment