Tuesday, June 10, 2014
SERIKALI,BUNGE WAKABANA KOO.
Do you like this story?
Kumekuwa
na mvutano mkubwa katika vikao vya mashauriano kati ya Serikali na Kamati ya
Bunge ya Bajeti, ambao pamoja na mambo mengine unaelezwa kuchangiwa na hatua ya
Serikali kukataa kuweka wazi vyanzo vya mapato kwa wajumbe wa kamati hiyo.
Kutokana
na hali hiyo, majadiliano kuhusu mwelekeo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa
fedha 2014/15, yamejikita katika makadirio ya matumizi pekee ambayo ni Sh19
trilioni, bila kufafanua fedha hizo zinatarajiwa kutoka katika vyanzo vipi.
Habari
kutoka ndani ya vikao hivyo zinasema mvutano baina ya timu ya Serikali
inayoongozwa na Waziri wa Fedha, Saada Nkuya Salum kwa upande mmoja na Kamati
ya Bajeti inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge ni
dhahiri hakuna makubaliano ambayo yamefikiwa hadi sasa.
Wajumbe
wa kamati hiyo wamekuwa wakitaka kufahamu vyanzo vya mapato ili kujiridhisha
iwapo Serikali imezingatia ushauri wa Bunge kuhusu kuongeza vyanzo vipya,
badala ya kuongeza kodi katika vyanzo vilevile kila mwaka.
“Tunashangazwa
na makadirio ya matumizi ya Sh19 trilioni kwa mwaka ujao wa fedha wakati
wameshindwa (Serikali) kukusanya Sh18 trilioni na kusababisha upungufu wa fedha
katika bajeti ya sasa. Wakijitahidi watamaliza mwaka huu wa fedha (Juni 30),
wakiwa na upungufu wa zaidi ya Sh600 bilioni, sasa tunataka kujua ni vyanzo
gani vitatumika kupata hizo trilioni 19?”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI,BUNGE WAKABANA KOO.”
Post a Comment