Tuesday, June 10, 2014

SERIKALI,BUNGE WAKABANA KOO.


Kumekuwa na mvutano mkubwa katika vikao vya mashauriano kati ya Serikali na Kamati ya Bunge ya Bajeti, ambao pamoja na mambo mengine unaelezwa kuchangiwa na hatua ya Serikali kukataa kuweka wazi vyanzo vya mapato kwa wajumbe wa kamati hiyo.

Kutokana na hali hiyo, majadiliano kuhusu mwelekeo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2014/15, yamejikita katika makadirio ya matumizi pekee ambayo ni Sh19 trilioni, bila kufafanua fedha hizo zinatarajiwa kutoka katika vyanzo vipi.

Habari kutoka ndani ya vikao hivyo zinasema mvutano baina ya timu ya Serikali inayoongozwa na Waziri wa Fedha, Saada Nkuya Salum kwa upande mmoja na Kamati ya Bajeti inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge ni dhahiri hakuna makubaliano ambayo yamefikiwa hadi sasa.

Wajumbe wa kamati hiyo wamekuwa wakitaka kufahamu vyanzo vya mapato ili kujiridhisha iwapo Serikali imezingatia ushauri wa Bunge kuhusu kuongeza vyanzo vipya, badala ya kuongeza kodi katika vyanzo vilevile kila mwaka.

“Tunashangazwa na makadirio ya matumizi ya Sh19 trilioni kwa mwaka ujao wa fedha wakati wameshindwa (Serikali) kukusanya Sh18 trilioni na kusababisha upungufu wa fedha katika bajeti ya sasa. Wakijitahidi watamaliza mwaka huu wa fedha (Juni 30), wakiwa na upungufu wa zaidi ya Sh600 bilioni, sasa tunataka kujua ni vyanzo gani vitatumika kupata hizo trilioni 19?”


0 Responses to “SERIKALI,BUNGE WAKABANA KOO.”

Post a Comment

More to Read