Thursday, June 12, 2014
CRISTIANO RONALDO NA WACHEZAJI WENZAKE KILA MTU AMEPEWA CHUMBA CHAKE, ARGENTINA WAWILI WAWILI
Do you like this story?
Chumba cha kulala: Nyota wa Ureno, Joao Moutinho ameposti picha hii kwenye mtandao wa Twita akionesha chumba chake cha kulala nchini Brazil. |
WAKATI
kitu cha kwanza atakachokiona Lionel Messi kila aamuka asubuhi ni mchezaji
mwenzake Sergio Aguero baada ya wawili hao kupangiwa chumba kimoja cha kulala,
Cristiano Ronaldo kwake ni tofauti kwani ataishia kuiona picha yake
kufuatia kupewa chumba cha peke yake.
Pengine
hili litakuwa jambo jema kwa Ronaldo aliyeshangilia bao la nne la Real Madrid
kwenye fainali ya UEFA baina ya Real Madrid dhidi ya Atletico Madrid kwa kuvua
jezi yake na kutunisha kifua chake.
Ureno
waliwasili katika kambi yao na kukuta wameshaandaliwa vyumba vya kulala vikiwa
na majina ya wachezaji na kikosi kwenye vitanda vyao, pia kumewekwa picha zao
ukutani.
Kiungo
Joao Moutinho na beki Joao Pereira wote kwa pamoja wameposti picha za vyumba
vyao kwenye mtandao wa Twita na Instagram wakifurahia kabla ya kucheza mchezo
wao wa ufunguzi wa kundi D dhidi ya Ujerumani mjini Salvador juni 16.
Licha
ya wasiwasi uliotanda juu ya Ronaldo kukivaa kikosi cha Joachim Low baada ya
kusumbuliwa na majeruhi ya mguu aliyoipata kwenye mechi za UEFA, nyota huyo
mwenye miaka 29 ameonekana kuimarika hasa baada ya kucheza kwa dakika 66 kwenye
ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Ireland siku ya jumatano.
Baada ya
mechi ya Ujerumani, vijana wa Paulo Bento watakabiliana na Marekani juni 22
mjini Manaus, kabla ya kucheza mechi ya mwisho ya makundi mjini Brasilia dhidi
ya Ghana juni 26.
Hoteli ya
Argentina kwenye kombe la dunia ilipangwa mapema wiki hii, huku ikionesha
wachezaji gani watakuwa wanalala chumba kimoja wakati wote wa mashindano.
Mpangilio
unaonesha kuwa washambuliaji Messi na Aguero watakuwa wanalala chumba kimoja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “CRISTIANO RONALDO NA WACHEZAJI WENZAKE KILA MTU AMEPEWA CHUMBA CHAKE, ARGENTINA WAWILI WAWILI”
Post a Comment