Friday, June 6, 2014
JOSE MOURINHO AVUTIWA NA FABREGAS, PIQUE ASEMA `DILI` LIMEKAMILIKA KWA PAUNDI MILIONI 26.8
Do you like this story?
![]() |
| Amekiri:Bosi wa Chelsea. Jose Mourinho amesema klabu yake inavutiwa kumsajili nyota wa zamani wa Asernal. |
![]() |
| Dili limekamilika: Cesc Fabreagas amehamia Chelsea, kwa mujibu wa mchezaji mwenzake wa Hispania Gerard Pique. |
![]() |
| Mchezaji mwenzake? Fabregas anaweza kujiunga na mshambuliaji wa Hispania Diego Costa katika dimba la Stamford Bridge msimu ujao. |
KOCHA
`mbwatukaji` Jose Mourinho amekiri kuwa Chelsea inavutiwa kumsajili Cesc
Fabregas kutoka klabu ya FC Barcelona, huku mchezaji mwenzake wa Hispania
Gerard Pique amesema dili hilo limekamilika kwa paundi milioni 26.8.
Kocha huyo
amesema kuwa ni wazi Fabregas anataka kurudi ligi kuu ikiwa ni miaka mitatu
imepita tangu aondoke Asernal, hivyo anafuatilia kwa makini ili kumsajili baada
ya kombe la dunia.
Wakati huo
huo Chelsea wako tayari kumpa ofa ya mshahara wa paundi milioni laki mbili kwa
wiki winga wao hatari, Eden Hazard ili kuwaziba mdomo Paris Saint-Germain
wanaoiwinda saini yake.
Juu ya
kiungo wa Hispania, Mourinho alisema: "Kwa kiasi fulani tunavutiwa na
Fabregas. Ninafuatilia hali halisi. Inaonekana yuko tayari kuondoka Barcelona
na anavutiwa kurudi England. Hili liko wazi. Lakini sio leo wala kesho au kabla
ya kombe la dunia".
"Kuna
mchakato huko anakotaka kuondoka, anataka kuja England kwasababu ni taifa
analopenda kucheza. Tunavutiwa kufuatilia hali halisi".
Wakati huo
huo, Pique kwa upande wake anasema dili hilo limekalimika. Beki huyo wa
Hispania alinaswa na Kamera mjini Washington akimwambia kocha wa Hispania ,
Vicente del Bosque kuwa Fabregas ataondoka Barcelona kwa dau la paundi
milioni 26.8 baada ya klabu hiyo kumalizia msimu bila kikombe.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)




0 Responses to “JOSE MOURINHO AVUTIWA NA FABREGAS, PIQUE ASEMA `DILI` LIMEKAMILIKA KWA PAUNDI MILIONI 26.8”
Post a Comment