Thursday, June 12, 2014
SINA MPANGO WA KUMUUZA HAZARD - MOURINHO.
Do you like this story?
MENEJA
wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amepuuza tetesi zilizozunguka mustakabali wa
Eden Hazard na kudai kuwa hawezi kumruhusu nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji
kuondoka katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi.
Hazard
mwenye umri wa miaka 23 amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda kwa mabingwa wa
Ufaransa, Paris Saint-Germain huku kocha wake Laurent Blanc akidai hadharani
kwamba anamuhitaji mshambuliaji huyo.
Pamoja
na kutofurahishwa na kiwango cha Hazard wakati wa msimu uliopita wa Ligi Kuu,
Mourinho sasa amethibitisha kuwa hana mpango wowote wa kumuachia nyota huyo wa
zamani wa Lille.
Mourinho
amesema kwasababu alisema Hazard hana kila anachotakiwa kuwa nacho mshambuliaji
hajamaanisha kwamba alikuwa hamuhitaji mchezaji huyo kwani bado ataendelea
kuwepo katika mipango yake katika siku nyingi zijazo atakazokuwepo Chelsea. Hazard
ni mfungaji anayeongoza kwa mabao kwenye timu hiyo msimu uliopita akiwa
amefunga mabao 14 na kutoa usaidizi mara saba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SINA MPANGO WA KUMUUZA HAZARD - MOURINHO. ”
Post a Comment