Thursday, June 12, 2014
MAZOEZI YA ARGENTINA YAVAMIWA NA RONALDINHO `FEKI`, MESSI APIGIWA MAGOTI NA KUFUTWA VIATU...HATARI!
Do you like this story?
Nakujua wewe! Shabiki anayeonekana kama Ronaldinho alivamia mazoezi ya Argentina kwenye uwanja wa Belo Horizonte |
Nyota akigoma kutoka: Messi akifurahia wakati shabiki akitolewa na maofisa, kufafana na Ronaldinho kulimfanya Messi acheke sana |
Messi aliamua kumkumbatia jamaa. |
Shabiki akifuta kiatu cha kulia cha Lionel Messi baada ya kuvamia uwanjani wakati wa mazoezi |
MAZOEZI ya
Argentina jana jumatano yalivamiwa na mtu moja mwenye sura inayofahamika
duniani.
Wakati
Lionel Messi na wachezaji wenzake wakijiandaa kuelekea mchezo wa ufunguzi wa
kundi lao dhidi ya Bosnia siku ya jumapili, shabiki mmoja mwenye sura
inayofanana na nyota wa zamani wa Brazil, Ronaldinho alivamia uwanjani.
Waargentina
walimfurahia jamaa huyo lakini alitolewa na maofisa wa uwanja.
Mashabiki
wengi walivamia uwanjani na kumpigia magoti nahodha huyo wa Argentina, Lionel
Messi huku wakifuta viatu vyake.
Messi
alicheka tu na aliwakumbatia mashabiki hao na alimpa shabiki mmoja sweta lake
kabla ya walinzi kumtoa.
Mashabiki wengine waliukimbilia
mpira ambao Muargentina huyo alikuwa anautumia katika mazoezi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MAZOEZI YA ARGENTINA YAVAMIWA NA RONALDINHO `FEKI`, MESSI APIGIWA MAGOTI NA KUFUTWA VIATU...HATARI!”
Post a Comment