Thursday, June 12, 2014
WATU 10 WATIWA MBARONI NA POLISI KUFUATIA VURUGU ZILIZOTOKEA JIJINI MWANZA
Do you like this story?
Polisi jijini Mwanza imelazimika
kutumia mabomu ya machozi kufuatia vurugu za baaadhi ya wafanyabiashara wadogo
maaarufu kama machinga na watoto wa mitaani wakipinga kupinga zoezi la
kuhamishwa eneo la Makoroboi walilokuwa wakifanyia biashara hapo awali.
Zoezi hili limesababisha wafayabiashara
mbalimbali kufunga biashara zao na wengine kupoteza mizigo kutokana na vurugu
hizo huku idadi kubwa ya wananchi wakishindwa kuendelea na shuguli zao
Nia aina ya vurugu zilizo tokea kwa
takribani masaa matano katikati ya jiji la Mwanza baada ya halmashauri ya jiji
kulazimika kuvunja vibanda vya wafanya biashara wakidai kukaidi agizo la mpango
wa kusafisha jiji.
Vurugu hizi zimelazimu wafanyabiashara
wote jijini hapa kusitisha utoaji wa huduma za kibiashara kwa wananchi
Baadhi ya Wamachinga katika eneo la
makoroboi waliungwa mkono na watoto wa mitaani jambo lilowapa wakati mgumu
jeshi la polisi katika kuthibiti vurugu zilizodumu kwa muda
Ilikuwa ni vigumu kwa mwananchi kuingia
na kutoka katikati ya jiji, wakihofia usalama wa maisha yao, waliokuwa maeneo
ya vurugu walilazimika kufungiwa ndani ya soko na katika maeneo mengine ili
kulinda usalama.
Mwenyekiti wa wamachinga mkoa wa Mwanza
Joseph Mwita amekana kuhusika kwa wamachinga katika vurugu hizi na kuwahusisha
vijana wasio na kazi kutumia mwanya huu kuleta vurugu ili kupora vitu
mbalimbali kutoka kwa wafanya biashara na wananchi
Licha ya jeshi la polisi kufanikiwa
kuthibiti vurugu hizi kwa kutumia nguvu ya ziada mkiwemo vilungu halmashauri
yajiji la Mwanza imesisitiza kuwa zoezi hili ni endelevu.
Katika haatua nyingine kituo cha haki
za binadamu kimelaani kitendo hiki cha jeshi la polisi kutumia nguvu kupita
kiasi huku kikiitaka serikali kuwa na mpango madhubuti wa ajira kwa vijana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WATU 10 WATIWA MBARONI NA POLISI KUFUATIA VURUGU ZILIZOTOKEA JIJINI MWANZA ”
Post a Comment