Monday, July 14, 2014

ASHAURI OFISI ZA SERIKALI ZOTE KUHAMIA DODOMA ILI KUPUNGUZA MSONGAMANO.





Serikali  imeshauriiwa kuendeleza mchakato wa kuhamishia ofisi  zote zake  mkoani  Dodoma kwenye makao makuu ya nchi yetu ili  kuweza kupunguza msongamano wa watu na magari.
Hayo yalisemwa na Mtanzania Mzalendo, John Lyasenga wakati akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa mikutano Idara ya Habari (MAELEZO) jijini Dar es Salaam.

“ Kutokana na jiji la Dar es Salaam kuwa na msongamano  wa watu na foleni za magari, kuna umuhimu kwa  Serikali kufikiria suala hili la kuhamishia ofisi zake na huduma zingine muhimu kwa mji huo mkuu wa Tanzania kwa ni kwa kufanya hivyo  kutaleta fursa  kwa wakazi wa mji huo,”alisema  Lyasenga.

Aidha aliongeza kuwa  faida za kuhamia Dodoma  ni pamoja na kuwepo kwa fursa mbalimbali kama vile ajira ,kuongeza pato la mkoa kupitia ujenzi wa viwanda vitakavyoongeza uzalishaji na kupunguza  maafa kwa jiji la Dar es Salaam kama vile mafuriko kutokana na wingi wa watu.

Mkoa wa Dodoma ina ukubwa wa eneo 41,000 kilomita za mraba na idadi ya watu ni 2,083,588 kutokana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.

Aliongeza kuwa, hali ya hewa  ya mkoa huo ni nzuri,ukilinganisha na mkoa wa Dar es salaam wenye kilomita za mraba 1,397 huku hali ya hewa, ikiwa ni joto wastani na idadi ya watu  ikizidi kuongezeka  hadi kufikia milioni 4,364,541

0 Responses to “ASHAURI OFISI ZA SERIKALI ZOTE KUHAMIA DODOMA ILI KUPUNGUZA MSONGAMANO.”

Post a Comment

More to Read