Tuesday, September 2, 2014
NYOTA WALIOVUNA FEDHA NYINGI USAJILI 2014/15
Do you like this story?
Shomari Kapombe -Azam FC |
Frank Domayo - Azam |
Kama
ilivyozoeleka katika kila kipindi cha usajili, wapo wachezaji watakaotawala
mazungumzo ya wapenzi wa soka kutokana na usajili wao kuzigharimu fedha nyingi
klabu zao mpya na wakati mwingine klabu za awali.
Jambo hili
hutokea katika ligi za nchi mbalimbali duniani kote zikiwamo zile zenye
umaarufu kama vile Ligi Kuu England, Hispania (La Liga) , Italia (Serie A) na
Ujerumani (Bundesliga).
Mara zote
wachezaji wanaonunuliwa kwa fedha nyingi kipindi cha usajili ni wale
walioonyesha viwango vya juu na kuwa tegemeo kwa klabu zao msimu uliotangulia.
Kwa kifupi,
kipindi cha usajili ni kipindi cha neema kwa wachezaji binafsi, pia kwa klabu
zao zinazowamiliki kutokana na kupata fedha nyingi kulingana na thamani wanayoonyesha
ndani ya uwanja.
Kwenye kipindi
cha usajili wa wachezaji kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara
utakaoanza Septemba 20, pia unawakuta wachezaji walioacha historia kwa kuvuna
fedha nyingine kupitia mikataba mipya.
Ifuatayo ni
orodha ya wachezaji walionunuliwa kwa fedha nyingi na kuacha historia kwenye
dirisha la usajili kwa ajili ya msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2014/15:
Shomari
Kapombe -Azam FC (Sh105 milioni)
Beki Shomari
Kapombe aliweka rekodi ya kuwa mchezaji mzalendo aliyesajiliwa kwa fedha nyingi
wakati Azam FC ilipomnunua kutoka timu ya daraja la nne ya As Cannes ya
Ufaransa.
Inadaiwa kuwa
Azam ilimnunua Kapombe ambaye pia ni beki wa zamani wa Simba baada ya ‘kuvunja
benki ‘kwa kuipa AS Canes kitita cha Sh 105 milioni.
Awali rekodi
hiyo ilikuwa inashikiliwa na kiungo mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa ambaye
mwaka 2010 alihamia Azam kutoka klabu hiyo ya Jangwani kwa dau la Sh 98
milioni.
Frank
Domayo - Azam (Sh70 milioni)
Hakuna ubishi
kwamba kiungo huyu wa zamani wa Yanga ndiye mchezaji ambaye usajili wake
ulijadiliwa zaidi na wapenzi wa soka hasa wa Yanga baada ya kusajiliwa na Azam
FC kwa dau la Sh 70 milioni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “NYOTA WALIOVUNA FEDHA NYINGI USAJILI 2014/15”
Post a Comment