Thursday, January 8, 2015
KIJANA ‘AJISALIMISHA’ KUHUSIANA NA SHAMBULIO LA KIGAIDI UFARANSA.
Do you like this story?
Mtuhumiwa Cherif Kouachi (kushoto) na ndugu yake Said Kouachi. |
Polisi wakiendesha oparesheni ya kuwakamata watuhumiwa katika kitongoji cha Croix-Rouge eneo la Reims, kaskazini mwa Ufaransa. |
Polisi wakilinda jengo moja huko Reims wakati wapelelezi wakiendesha shughuli zao kuhusiana na shambulio hilo la kigaidi. |
NDUGU wawili na kijana mmoja jana walielezewa kuwa ndiyo watuhumiwa
watatu wanaohusishwa na shambulio la kigaidi jana dhidi ya jarida lenye kupinga
Uislam nchini Ufaransa liitwalo Charlie Hebdo mjini Paris ambapo watu 12
waliuawa na saba kujeruhiwa.
Miongoni mwa
waliouawa ni pamoja na mhariri mkuu, wachoraji wanne wa vikatuni na
polisi wawili.
Inasemekana
sababu ya kuvamiwa kwa ofisi za jarida hilo ni kuchapisha vikatuni vyenye
kukashifu dini ya Kiislam. Washambuliaji hao walitoroka baada ya
shambulio hilo.
Watuhumiwa
hao ni Said Kouachi (34), Cherif Kouachi (32) wote wakazi wa jiji la
Paris, ambao ni pamoja na Hamyd Mourad (18) kutoka mji wa kaskazini-mashariki
wa Reims, Ufarransa, aliyejisalimisha polisi baada ya kuona katika vyombo vya
habari alikuwa anatafutwa.
Hivi sasa
polisi wanawatafuta ndugu hao wawili katika eneo la Croix Rouge hulo Reims.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KIJANA ‘AJISALIMISHA’ KUHUSIANA NA SHAMBULIO LA KIGAIDI UFARANSA.”
Post a Comment