Wednesday, January 7, 2015
CITY KUWAVAA ‘WAMALAWI’ JUMAMOSI.
Do you like this story?
Mbeya
City FC inayoonolewa na Kocha Bora wa msimu uliopita, Juma
Mwambusi, Jumamosi Junuari 10 itacheza mechi wa kirafiki dhidi ya Karonga
United ya Malawi. mechi ya kirafiki itakayochewzwa wilayani kyela.
Kwa
mujibu wa waandaji wa mchezo huo Chama cha Soka Kyela, kiingilio
kimepangwa kuwa Sh. 1000 ili kuwawezesha mashabiki wengi kujitokeza
kuona mchezo huo wa kirafiki wa kimataifa.
Mwambusi
amesema atauchukulia mchezo huu kama kipimo kwa vijana wake kuelekea
mchezo wa ligi kuu ya Vodacom dhidi ya Kagera Sugar FC utakaopigwa Uwanja wa
CCM Kirumba Januari 17, kufuatia kuahirishwa kwa michezo yao miwili dhidi ya
Simba na Yanga zilizokwenda Zanzibar kushiriki Kombe la Mapinduzi.
“Ni
jambo zuri kupata mechi ya kirafiki ya kimataifa katika wakati huu,
tutauchukulia mchezo huu kama kipimo muhimu kuelekea mchezo wa ligi dhidi ya
Kagera Sugar hasa ukizingatia kuwa Karonga ni timu inashiriki ligi kuu huko
Malawi.
"Wote
tunafahamu uwepo wa michauano ya Kombe la Mapinduzi umefanya kuahirishwa
kwa michezo yetu miwili iliyokuwa tucheze, hilo halijatuvunja moyo ndiyo maana
nasema hiki ni kipimo kizuri tukijiandaa kwenda kucheza mchezo mwingine wa ligi
huku lengo letu likiwa ni kupata matokeo mazuri,” amesema Mwambusi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ CITY KUWAVAA ‘WAMALAWI’ JUMAMOSI.”
Post a Comment