Wednesday, January 7, 2015
TASAF KUTUMIA MIKUTANO YA HADHARA KATIKA MITAA NA VIJIJI KUTAMBUA KAYA MASKINI KATIKA MPANGO WA AWAMU 3.
Do you like this story?
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bw Abbas Kandoro akizungumza na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Tasaf |
Kaimu Mkurugenzi wa Tasaf Taifa, Zuhura Mdungi akisoma Taarifa ya utekelezaji. |
WAshiriki wa Warsha ya kujenga uelewa kuhusu mpango wa kunusuru kaya maskini kwa viongozi, watendaji na wawezeshaji |
Mikutano ya hadhara ya
vijiji na mitaa inatarajia kutumika katika kuwatambua walengwa wa mpango wa
kuzisaidia kaya masikini unaotekelezwa na mfuko wa maendeleo ya jamii
(TASAF)awamu ya Tatu.
Akizungumza katika
uzinduzi wa mpango huo katika halmashauri ya jiji la Mbeya mwakilishi wa
mkurugenzi mtendaji wa Tasaf,Zuhura Mdungi alisema kuwa njia hiyo ya mikutano ya hadhara itasaidia
kuwapata walengwa sahihi wa mpango huo.
Alisema Kuwa katika
mikutano hiyo wanakaya wenyewe ndiyo watahusika katika kuwatambua na
kuwateua watu ambao wapo katika kaya
masikini waliopo katika maeneo husika ili kuondokana na migongano wakati wa
utekelezaji wa mpango huo
Mdungi alisema kuwa
malengo ya mpango huo ni kuziwezesha
kaya masikini kuongeza matumizi muhimu kwa njia endelevu,kuwekeza katika
rasilimali watu hususani watoto kwa
kuwajenga na kuweza kupata elimu bora,chakula
na kuongeza kipato kwa kupitia uwekaji wa akiba na shughuli za kiuchumi ili
kuboresha maisha.
Alisema kuwa mpango huo
pia utakuwa unatoa ajira kwa kaya masikini zenye watu wenye uwezo wakufanya
kazi wakati wa mjanga mbali mbali kama ukame na mafuriko na kwamba pia mkakati
huo umelenga kupunguza mazingira hatarishi kwa kipindi cha kati na kirefu kwa
kuwekeza kwewnye elimu,na lishe kwa watoto.
Akizindua mpango huo
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amewataka viongozi na watendaji kutekeleza
mpango huo kwa misingi ya kisiasa kwa kutokuwa na upendeleo katika kutambua
kaya masikini.
“Acheni watu watambuane
wenyewe na mpango huu usiwe wa kificho wala sisi vbiongozi tusiwe na upendeleo
na lisiwe na misingi ya kisiasa hivyo kila mmoja atomize wajibu wake kwa
uwazi”alisema
Utekelezaji wa mpango
wa kunusuru kaya masikini unatarajia kuzifikia kaya 1milioni zenye watu
7milioni kwa miaka kumi katika awamu mbili za miaka mitano kwa kila awamu.
Mwisho
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “TASAF KUTUMIA MIKUTANO YA HADHARA KATIKA MITAA NA VIJIJI KUTAMBUA KAYA MASKINI KATIKA MPANGO WA AWAMU 3.”
Post a Comment