Thursday, January 8, 2015
MADAKTARI WASHIRIKIANA KUOKOA MAISHA YA MAPACHA WALIOUNGANA.
Do you like this story?
Timu ya madaktari wa watoto katika hospitali ya rufaa ya Bugando
wameungana ili kuokoa maisha ya mapacha walioungana. Mapacha hao
wamezaliwa na Elena Paulo, mwenye umri wa miaka 20, Januari 3, mwaka huu katika
hospitali ya hospitali ya mkoa ya Mara na baadaye kuhamishiwa
katika hospital ya rufaa ya Bugando mkoani Mwanza kwa ajili ya matibabu
zaidi.
Watoto hao walikuwa na uzito wa kilo 4.6 kwa pamoja wakati walipozaliwa
na walikuwa wameungana vifua na matumbo.
Kwa mujibu wa Dk Festo Manyama, daktari wa watoto hospitali ya rufaa ya
Bugando, timu ya madaktari wa upasuaji na wataalamu wengine wamekusanyika
kuamua namna bora ya kukabiliana na hali yao. "tunafanya kila liwezekanalo
katika uwezo wetu ili kuokoa maisha ya watoto hawa'," alisema.
Alisema kabla ya upasuaji, mapacha hao walitakiwa kupitia
tomografia (CT) na kufanya kipimo kijulikanacho kama Ultra sound ili
kujua kama watoto hao wameungana baadhi ya maeneo na viungo
muhimu.
"Tumeshafanya kipimo cha Ultra Sound na kupata matokeo yanayoonyesha
kuwa hakuna sehemu nyingine muhimu walizoungana, lakini tunahitaji
kufanya vipimo vingine kwa kutumia mashine ya CT scan, ambayo itatupatia
hitimisho, "alisema Manyama.
Alisema madaktari wataweza kufanya upasuaji endapo watoto hao
hawatakuwa wameungana sehemu muhimu katika miili yao.
Kwa mujibu wa Dk Manyama, watoto hao wawili wanahitaji ufuatiliaji wa
karibu wa daktari ili waweze kuepukana na magonjwa. "tuwapa dawa na
kuwalinda na magonjwa ya kuambukiza, pia wanatumia mashine ya oksijeni kwa
kupumua na mirija ya chakula", anaongeza Dr Manyama.
Aliongeza kuwa uongozi wa hospitali hii inatazamia kutoa rufaa ili watoto
hawa wapelekwe Hospitali ya Taifa Muhimbili. "Tutawahamishia hospitali ya
muhimbili kwa sababu hospitali yetu haina uwezo mkubwa wa kukabiliana na kesi
hii, lakini kwa wakati tunafanya kila tuwezalo ili kuokoa maisha yao."
Alisema.
Mama wa mapacha hao, Bi Elena Paulo aliwaomba serikali kumuunga mkono ili
kuhakikisha watoto wake wanapata huduma ya afya bora inayohitajika katika hali
yao.
"Hofu yangu kubwa ni kwamba hospitali zetu hawataweza kukabiliana na
hili, nimeambiwa upasuaji unaweza kufanyika nje ya nchi na Mimi ni mama maskini
hivyo ninaomba serikali inisaidie", alisema.
Tanzania imekuwa ikishuhudia matukio kadhaa ya mapacha walioungana katika
miaka ya hivi karibuni. Mwishoni mwa
mwaka jana hospitali ya Apollo imetangaza kufanikiwa kutenganisha mapacha
waliokuwa wameungana kutoka Tanzania katika upasuaji ambayo ulichukua
masaa 11 na wataalamu 50.
Mapacha Abriana na Adriana walikuwa wameungana katika kifua chini ya
tumbo, hali ya kitaalamu inajulikana kama 'Thoraco Omphalopagus'. Mapacha hao
walitenganishwa baada ya mipango ya kina na ushirikiano kati ya
madakitari bingwa wa mfumo wa mkojo, figo ini na moyo na madakitari
bingwa wa watoto na kuteua dakitari bingwa mmoja kama kiongozi wa timu ambaye
alisimamia utaratibu mzima wa upasuaji.
Mapacha hao waliokuwa wameungana kuanzia chini ya kifua na tumbo,
halikadhalika walikuwa wakitumia mvungu mmoja wa moyo na walikuwa wameungana
Ini.
Upasuaji huu wa mafanikio wa kutenganisha mapacha walioungana kutoka
nchini Tanzania sio wa kwanza kufanywana hospitali ya Apollo. Mwishoni mwa
mwaka 2013 mapacha wengine wakiume waliokuwa wameungana wajulikanao kitaalamu
kama Pygopagus, Ericana na Eluidi kutoka Tanzania walifanikiwa kutenganishwa
nawataalamu wa hospitali hiyo. Matukio amabayo yamepandisha chati nakuipa hadhi
ya juu hospitali ya Apollo iliyopo nchini India kwa ujumla kama kiongozi katika
sekta ya afya na mfano wakuigwa na nchinyingine ikiwemo Tanzania. Hospitali
hiyo inamahusiano mazuri na nchi ya Tanzania na imekuwa ikipokea idadi
kubwa ya wagonjwa kutoka nchini Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MADAKTARI WASHIRIKIANA KUOKOA MAISHA YA MAPACHA WALIOUNGANA.”
Post a Comment