Monday, February 23, 2015
HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA YAWAKUMBUKA WAHANGA WA JANGA LA MVUA.
Do you like this story?
Wakazi wa Mtaa wa Ilemi juhudi jijini Mbeya wakiwa tayari kukabidhiwa msaada huo. |
Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya Quip Mbeyela akizungumza katika makabidhiano ya Msaada huo. |
Kaimu Mkurugenzi jiji la Mbeya Dkt Samwel Lazaro akizungumza kabla ya kukabidhi msaada huo kwa waathirika wa janga hilo.Picha na David Nyembe Fahari News |
(Picha na Fahari News)
Halmashauri
ya jiji la Mbeya imetoa msaada kwa Wananchi wa Mtaa wa
Ilemi jijini Mbeya kufuatia mvua
kubwa iliyoambatana naupepomkali kunyesha na kuharibu nyumba zaidi ya 40 huku Kaya 38 zikikosa makazi.
Akizungumza
wakati wa kukabidhi msaada huo Kaimu Mkurugenzi Halmshauri ya jiji la Mbeya
Dkt Samwel Lazaro amesema baada ya kupata taarifa za janga hilo uongozi wa
halmashauri hiyo ulikaa na kujadiliana namna ya kutoa msaada kwa waathirika
hao.
Amesema
katika majadiliano hayo uongozi huo ulikubaliana na kuamua kutoa
mchango wao ambao Sukari kilo 3 kwa kila kaya pamoja na Unga wa ugali mfuko
mmoja wa kilo 10 na Maharagwe kilo 1.
Amesema
pamoja na kutoa msaada huo lakini pia uongozi wa halmshauri hiyo umeanza
mchakato wa kufanya tathimini
ili
kutambua hali halisi ya uhalibifu huo.
|
Aidha
Dkt Lazoro amesema kuwa kutokana na baadhi ya miundo mbinu ya shule ya Msingi
Ilemi kuharibiwa kwa kuezuliwa mapaa yake pamoja na vyoo tayari mafundi
wamekwisha anza utaratibu wa kufanya ukarabati kwa gharama za serikali pasipo
kuwa husisha wananchi .
Mvua
hizo zilizo nyesha hivi karibuni jijini hapa zilileta madhara hayo kwa kuharibu
baadhi ya miundo mbinu ya shule ya msingi Ilemi pamoja na kuharibu makazi ya
watu kwa kaya zaidi ya 38 na kupelekea wakazi hao kukosa mahali pa kuishi
pamoja na kuhitaji msaada wa maradhi mbalimbali.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA YAWAKUMBUKA WAHANGA WA JANGA LA MVUA.”
Post a Comment