Monday, February 23, 2015
KAPOMBEA APIGIA ‘SALUTI’ MUZIKI WA PRISONS
Do you like this story?
MCHEZAJI kiraka wa Azam fc, Shomari
Salum Kapombe amesema matokeo mabaya wanayopata Prisons ndio chanzo cha
kuwakazia jana usiku katika mechi ya ligi kuu Tanzania bara iliyomalizika kwa
suluhu uwanja wa Azam Complex.
“Prisons walifungwa mechi iliyopita na
Yanga, leo wamekuja na nguvu. Wameonesha kiwango kizuri na nidhamu ya mchezo.
Wamejilinda vizuri na kucheza mpira”.
“Tumejitahidi kufika mara nyingi golini
kwao, lakini kipa wao (Mohammed Yusuph) amekuwa imara”.
Kwa matokeo ya jana, Azam fc
wanaendelea kushika nafasi ya pili kwa pointi 27 baada ya kushuka dimbani mara
15, wakati Yanga wanaongoza msimamo kwa pointi 31 baada ya kucheza mechi 15.
Kapombe amesema baada ya mechi hiyo,
sasa wanaelekea macho yao katika mechi ya marudiano ya ligi ya mabingwa barani
Afrika dhidi ya Al Merreick.
Mechi ya kwanza Azam walishinda 2-0 na
mechi ya marudiano itayopigwa mwishoni mwa wiki hii, matajiri wa Dar wanahitaji
ushindi au kufungwa magoli yasiyozidi mawili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KAPOMBEA APIGIA ‘SALUTI’ MUZIKI WA PRISONS”
Post a Comment