Tuesday, February 17, 2015
KOCHA SIMBA SC ATUA AFC LEOPARDS YA KENYA.
Do you like this story?
Na Bertha Lumala, Dar
es Salaam
Ukimuona wa nini,
wenzako wanasema watampata lini! Aliyekuwa kocha mkuu wa Simba SC Mcroatia
Zdrvako Logarusic anatarajiwa kutua nchini Kenya wiki hii na kuanza kazi rasmi
ya kuinoa timu yakje mpya ya AFC Leopards.
Ijumaa, Leopards
walithibitisha kumteua Mcroatia huyo kuwa kocha mkuu wa timu yao akirithi
mikoba ya Mdachi, Pieter De Jongh ambaye amefukuzwa na klabu hiyo ya Ligi Kuu
ya Kenya.
Ingwe kupitia kwa
Katibu wake Timothy Lilumbi imethibitisha kwamba Logarusic, maarufu Loga atatua
nchini humo wiki hii na kuanza kazi rasmi.
"Tuko katika
hatua za mwisho za kumtumia Loga tiketi ya ndege, na tunatarajia kumuona nchini
ndani ya wiki hii. Ataanza kutekeleza majukumu ya timu mara tu baada ya
kuwasili," amesema.
Kocha huyo wa zamani
wa Gor Mahia amekaa bila timu tangu Agosti 2014 alipofukuzwa na uongozi mpya wa
Simba SC, chini ya Rais Evans Aveva kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutokana na
utovu wa nidhamu.
Akiwa Tanzania, Loga
alidaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na baadhi ya wasanii wa filamu, jambo
ambalo lilidaiwa kuuchafua uongozi wa Simba SC kwa vile kocha huyo alifikia
hatua ya kukacha mazoezi ya timu ili ale raha na mademu hao wa Bongo Movie.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KOCHA SIMBA SC ATUA AFC LEOPARDS YA KENYA.”
Post a Comment