Tuesday, February 17, 2015
PRISONS: TUMELAZIMISHWA KUCHEZA DHIDI YA YANGA SC ALHAMISI.
Do you like this story?
Kocha Mkuu wa Tanzania
Prisons, David Mwamaja amesema wamelazimishwa na Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF) kucheza mechi Alhamisi dhidi ya Yanga SC mjini Mbeya.
Mwamaja amesema kikosi
chake kilichokuwa kimeweka kambi jijini hapa kujiandaa kwa mechi ya mwishoni
mwa wiki hii dhidi ya mabingwa watetezi Azam FC, kimelazimika kurejea jijini
Mbeya baada ya kutakiwa kufanya hivyo na TFF.
Amesema kikosi chake
kimetua nyumbani, Mbeya leo jioni, tayari kuwavaa Yanga SC ambao wametamba moto
wao hauzimiki kwa sasa,
“Timu ilikuwa Dar es
salaam tukijiandaa kwa mechi dhidi ya Azam, lakini tumelazimishwa kurejea Dar
es Salaam kucheza dhidi ya Yanga," amesema kocha huyo aliyewahi kuinoa
Simba SC mwaka 1999 wakati Mtibwa Sugar FC wakitwaa taji la kwanza la Tanzania
Bara.
Mwamaja ambaye kikosi
chake kiko mkiani mwa msimamo, amesema hana hofu dhidi ya kikosi cha Yanga SC
kwa kuwa anakifahamu vyema.
"Yanga tunawajua na wao pia wanajua moto wetu. Tumekuwa
na matokeo ya sare nyingi, lakini sare si mbaya, bunduki zetu ziko sawa kwa
ajili ya mechi hiyo," amesema zaidi Mwamaja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “PRISONS: TUMELAZIMISHWA KUCHEZA DHIDI YA YANGA SC ALHAMISI.”
Post a Comment