Friday, February 20, 2015
MKUU WA KITUO CHA POLISI JELA MIAKA 30 KWA KUBAKA MAHABUSU HUKO NJOMBE
Do you like this story?
Mahakama
ya Hakimu Mkazi Mkoa ya Njombe, imemhukumu aliyekuwa mkuu wa kituo cha Polisi
Ilembula kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka
mtuhumiwa aliyekuwa ndani ya mahabusu.
Hukumu
hiyo ilitolewa na Hakimu Augustine Rwezile, baada ya mshtakiwa huyo James
Nyambenga kukiri kosa hilo mahakamani, ambapo mshakiwa huyo anadaiwa kumtoa
msichana huyo kwenye chumba cha mahabusu alikokuwa anashikiliwa na kumbaka.
Mwanamke
huyo ambae ni mhudumu wa bar alikuwa anashikiliwa kwenye mahabusu ya kituo
hicho kwa tuhuma za uzururaji.
Akisoma
hukumu hiyo Hakimu Rwezile amesema ushahidi uliotolewa na upande wa
mlalamikaji na vielelezo vya daktari aliyempima msichana huyo viliweza
kuithibitishia Mahakama kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ MKUU WA KITUO CHA POLISI JELA MIAKA 30 KWA KUBAKA MAHABUSU HUKO NJOMBE ”
Post a Comment